LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAUMINI NA VIONGOZI WA MADHEHEBU YA DINI MKOANI GEITA WATAKIWA KUHAMASISHA AMANI.

Waumini na Viongozi wa madhehebu mbalimbali Mkoani Geita wametakiwa kuhamasisha suala zima la amani ya Taifa na Upendo katika Makanisa yao na  jamii inayowazunguka kuhusu  uchaguzi na mchakato wa upatikana kwa Katiba Mpya.

Hayo yalisemwa juzi na Kamanda wa Umoja wa
vijana wa CCM wilaya ya Nyan’gwale Mkoani Geita Idd Kassim,  wakati wa  harambee ya ujenzi  wa kanisa la The Evangelistc Assembles of God Tanzania (EAGT).

Harambee hiyo iliyofanyika septemba 21 ilikuwa na  lengo la kukusanya shilingi Millioni 9,970,000 kwa ajili ya ujenzi wa kanisa  hilo ambapo kiasi cha pesa taslim kilichopatikana ni sh.Million 2,291,200 na mifuko 2 ya saruji huku ahadi ikiwa ni sh. Million 250,000  viti 7 na Mifuko 5 ya saruji.

Kassim alisema  waumuni wanatakiwa kuwa mfano mzuri wa kuigwa na kutokubali  kuoingiliwa kisiasa na wanasiasa wasiolitakia mema  taifa na kuchochea vurugu zisizo na faida kwa watanzania.
“Tutambue hii ni nchi yetu sote na tunajukumu la kuilinda amani na upendo uliopo, uendelee kuwepo”Alisema Kassim.

Aidha Kamanda Idd aliwataka vijana wa wilaya hiyo,  kujiajiri wenyewe ili waweze kujiletea maendeleo katika  familia zao na  kuepukana na janga la ukosefu wa ajira kwa vijana.

“Sisi kama vijana ni jukumu letu wote kijituma na kufanya kazi kwa biidii ili tusiwe mizigo katika familia zetu na kuwa mfano mzuri wa kuigwa”Alisema.
Na: Prisca Japhes.

No comments:

Powered by Blogger.