LIVE STREAM ADS

Header Ads

JAMII IVUNJE UKIMYA ILI KUFICHUA UKATILI DHIDI YA WATOTO.

Juhudi mbalimbali za kuhakikisha kwamba Ukatili dhidi ya Watoto katika jamii unatokomezwa bado zinahitajika miongoni mwa wanajamii, baada ya kubainika kwamba Watoto walio wengi wanapitia Vitendo mbalimbali vya Ukatili.

Mkoani Mwanza Ukatili dhidi ya Watoto unaelezwa kuibuka kila Kukicha huku jambo la Kushangaza likiwa ni kwamba, Watoto walio wengi wamekuwa wakitendewa Ukatili wa aina mbalimbali na wanafamilia wenyewe wakiwemo wazazi wao.

Katika Tukio la hivi karibuni ambalo lilitokea katika Kata ya Buhongwa, Msichana Naomi Wilson Mwenye Umri wa Miaka 14 ambae ni Mwanafunzi wa Kidato cha Kwanza katika Shule ya Sekondari Twihurumie iliyoko Kata ya Buhongwa Jijini Mwanza, ameelezea namna alivyonusurika kifo baada ya Mama yake Mzazi kummwagia mafuta ya taa na kisha kumchoma moto hali ambayo imemuachia majeraha katika maeneo mbalimbali ya mwili wake hususani Mikononi, Usoni na Shingoni.


Naomi anasema "nakumbuka siku ya tukio ilikuwa usiku majira ya saa mbili ambapo mama alianza kuniadhibu na hatimae kumwagiza mafuta ya taa na kiberiti kijana wetu wa kazi na kisha kunichoma moto kwa kosa la kunikuta nje usiku huo nikiwa na kijana mmoja ambae ni rafiki yake na kaka".

Naomi anasema baada ya Mama yake kumtendea ukatili huo, alitorokea kusikojulikana na hadi sasa inaelezwa kuwa Mama Naomi hajulikani alipo ambapo baada ya tukio hilo Naomi alifikishwa katika Hospital ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure kwa ajili ya Matibabu zaidi.

Kwa sasa Naomi anauguza Majeraha yake katika Kituo cha Kuzuia na Kutokomeza Ukatili dhidi ya Watoto Majumbani lililopo Kiloleli Mkoani Mwanza la Foundation Karibu Tanzania, ambapo kiu kubwa ya Naomi anasema kuwa anatamani sana kuonana na mama yake kwa kuwa amekwisha msamehe na amemkumbuka sana Mama yake pamoja na mdogo wake.

Hatimae Radio Metro Fm na Binagi Media Group ilifika katika Ofisi za Shirika hilo la Kuzuia na Kutokomeza Ukatili la Foundation Karibu Tanzania ambapo mtoto Naomi anaishi kwa sasa huku akiendelea kuuguza majeraha ya moto aliyoyapa baada ya kuchomwa moto na mama yake mzazi na kuzungumza na Mariagoreth Itovelo ambae ni Afisa Ustawi wa Shirika hilo ambae alibainisha kwamba hali ya Naomi inaendelea vyema tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

Itovelo akaeleza kwamba Walifika katika Hospitali ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure Agost 13 mwaka huu ambapo Naomi alikuwa amelazwa kwa ajili ya Matibabu, ambapo alitibiwa na kuruhusiwa kutoka Hospitalini Agost 24 mwaka huu na kuelekea nyumbani kwao Buhongwa kabla ya kuchukuliwa na Shirika hilo Agost 28 mwaka huu baada ya Naomi kuwa na wasiwasi wa kuishi nyumbani kwao akihofia huenda mama yake angerudi na kumtendea ukatili zaidi.

Katika hatua nyingine Itovelo anatoa ushauri kwa wanajamii kujenga dhana ya mtoto wa mwenzio ni wako pia na hatimae kuvunja Ukimya na kufichua matendo ya Ukatili kwa watoto ambapo anawaasa wanajamii kufikiria mara mbili kabla ya kutenda ukatili wa aina yoyote dhidi ya watoto.
                                
Nae Abimelick Richard ambae ni Mwanasheria na Mwezeshaji wa Shirika la Foundation Karibu Tanzania anasema kuwa bado kuna kasi kubwa ya matukio ya Ukatili dhini ya Watoto katika jamii, hivyo Shirika hilo linajitahidi kutoa elimu kwa wanajamii ili kuweza kufichua na hatimae kutokomea Ukatili dhini ya watoto huku akibainisha kuwa kadri Shirika hilo linavyozidi kutoa elimu katika jamii ndivyo matukio mengi ya ukatili yanavyoripotiwa kwa kuwa hapo awali matukio mengi ya Ukatili katika jamii yalikuwa hayaripotiwi.
                                      
Katika hatua nyingine Richard anasema kuwa Shirika hilo linafanya kazi chini ya Kaulimbiu ya Vunja Ukimya, Fichua Ukatili hivyo wanajamii wanapaswa kuwa tayari kuchukia vitendo vya Ukatili dhini ya Watoto ambavyo anasema kuwa kwa asilimia kubwa vimewasababishia watoto walio wengi kupoteza viuongo vya miili yao, huku akibainisha kuwa katika kipindi cha miaka miwili iliyopita Shirika hilo limepokea taarifa za zaidi ya 250 za ukatili mkubwa dhidi ya watoto huku watoto zaidi ya 2,000 wakiwa wameokolewa baada ya shirika hilo kuingilia kati matukio ya ukatili waliyokuwa wakitendewa katika jamii.

Hakika ni jukumu langu, wewe pamoja na yule katika kuhakikisha kwamba vitendo vya Kikatili vya aina yoyote ile havikubaliki katika jamii, ambapo kubwa zaidi wanajamii wanaasa kuvunja ukimya na Kufichua Vitendo vya kikatili dhidi ya watoto na hatimae jamii nzima kwa lengo la kuwa na Familia Salama na Jamii Salama pia.

No comments:

Powered by Blogger.