Taa za Kuongoza Magari zilizowekwa katika eneo la Buzuruga Jijini Mwanza.
Akizungumzia
uwepo wa Taa za kuongoza magari katika eneo hilo la Buzuruga, Dede Petro Dede
ambae ni Mwenyekiti wa Chama cha Madereva Kanda ya Ziwa amesema kuwa, suala la
uwepo wa taa katika eneo hilo linapaswa kuangaliwa upya ikiwa ni pamoja na
kuboresha kwanza miundomindu ya barabara katika eneo hilo.
Amesema
uwepo wa taa hizo umesababisha foleni kubwa kinyume na matarajio yaliyokuwa
yamekusudiwa hivyo ili kuondoa usumbufu huo ni vyema barabara hiyo ikapanuliwa
kwanza kabla ya kuruhusu matumizi ya taa hizo, lakini pia akasisitiza kwamba
TANROADS inapaswa kuweka alama kwa ajili ya wananchi wanaovuka barabara kwa miguu
ili kuondoa usumbufu ambao wananchi wanaupata kwa hivi sasa.
|
No comments: