Akizungumza
katika Kikao hicho, Joseph Ngoseki ambae alimwakilisha Katibu Tawala Mkoa wa
Mwanza, alisema kuwa Serikali inafanya kila linalowezekana ili kuhakikisha kuwa
kunakuwepo na usawa kwa pande zote zinazohusika na biashara ya kazi za sanaa
kwa kufuata sheria na taratibu zilizopo kwa lengo la kuhakikisha kuwa wadau
wote wa kazi hizo wananufaika.
Nae Lutufyo
Mtafya ambae ni Afisa elimu, huduma kwa walipa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato
Mkoani Mwanza (TRA), alisisitiza zaidi juu ya uwepo wa mawasiliano ya karibu
baina TRA na wadau wote wa kazi za sanaa kwa lengo la kuhakikisha kwamba wadau
wote wanafanya shughuli zao kuwa kufuata taratibu ili kuondoa mkanganyiko
uliopo kwa wasambazaji na wauzaji wa kazi za sanaa ambao wanasema kuwa wamekuwa
wakifanya shughuli zao kwa mjibu wa sheria ikiwa ni pamoja na kulipia kodi
katika biashara zao.
|
No comments: