DENDEGO: CHANGAMKIENI FURSA ZA MWANAMKE NA UCHUMI.
Wanawake Wajasiriamali Mkoani Tanga wametakiwa kujitokeza na
kuchangamkia fursa zitakazotolewa na kampeni ya Mwanamke na Uchumi
inayotarajiwa kutolewa mwanzoni mwa mwezi ujao Mkoani Tanga ambapo zaidi ya
wanawake 300 watanufaika na mafunzo hayo yanayotolewa na kampuni ya Angels
Moment ya jijini Dar Es Salaam.
Mkuu wa
Wilaya ya Tanga Mh.Halima Dendego amesema fursa
zitakazotolewa ni fahari kwa wanawake na wajasiriamali wa mkoa huo kwani elimu
inahitajika sana wakati huu wa ushindani wa biashara.
“Fursa kama hizi mara
nyingi ni nadra kuzipata na Kampeni ya mwanamke na uchumi ni jibu la changamoto
mbalimbali kwa wajasiriamali kwani elimu watakayoitoa ni fursa pekee ya kusonga
mbele kibiashara na kiuchumi kwa wanawake wa mkoa wa Tanga” alisema.
Mkuu huyo wa wilaya amewaomba
Wadau mbalimbali waendelee kujitokeza kuunga mkono juhudi za Kampeni ya
mwanamke na uchumi kwani kupitia akina mama huduma zao zitaweza kufahamika na
kunufaika kwani ndiyo nafasi pekee ya kukutana na wajasiriamali na kusaidia
kuinua uchumi wa akinamama na Taifa kwa ujumla.
Kwa upande mwingine Mkurugenzi wa kampeni ya mwanamke na
uchumi Mahada Erick amesema kuwa kampeni ya mwanamke na uchumi ni jawabu la
changamoto zinazokumba biashara na ujasiriamali kwani elimu na semina
zitakazotolewa zitawapa msingi wa kuanza upya kuandaa biashara na ujasiriamali
kwa ujumla na pia kutoa hamasa kwa akinamama katika kujiletea maendeleo.
“ Kampeni hii inalenga kutoa hamasa na ari kwa akinamama kusonga
mbele kimaendeleo, Hakuna ubishi kuwa akinamama wana juhudi kubwa sana za
kutafuta fursa za kujiongezea kipato, ila tatizo ni elimu ya msingi ya
kuangalia fursa zinazowazunguka na jinsi ya kuendeleza biashara zao.”
Angels Moment itawakutanisha akinamama waliofanikiwa kibiashara na
ambao wanafanya ujasiriamali mbalimbali ili kuelezana mbinu mbalimbali za
mafanikio. Pia kutakuwa na wataalamu watakaotoa elimu ya ujasiriamali,
uwekezaji, uwekaji akiba na elimu ya afya’ anasisitiza.
Kampeni ya Mwanamke na uchumi Mkoani Tanga itafanyika tarehe tano
na sita mwezi ujaokatika Ukumbi wa Naivera
ambapo utapambwa na msanii Linah Sanga ambaye ni balozi wa Wanawake.Wadau
walioungamkono kampeni ya mwanamke na uchumi ni MKoani Tanga ni pamoja na
SSRA,NSSF,TBS,PSPF,GEPF,AGHAKHAN HOSPITAL,MINJINGUMAZAO,HSC, na NAIVERA COMPLEX.
Na:Christian Gideon, Angels moment.
No comments: