Ardhi inayopatikana Wilayani Tarime hakika haibagui, mbali ya zao la Mahindi pia mazao kama Matikiti Maji pia hulimwa na kustawi vyema.Huyu ni mmoja wa wakulima wa siku nyingi kutoka Kitongoji cha Chira, Kijiji cha Kenyamanyori Wilayani Tarime ambae anafahamika kwa jina la Zakaria Isanchu.Anasema kwake yeye Kilimo ni kila kitu na amekuwa akilima mazao mbalimbali ikiwemo Mahindi, Mtama, Mhogo, Tikiti Maji, mazao ya mboga mboga, Matango, nyanya na mengine mengi kulingana na Neema ya ardhi inayopatikana Wilayani Tarime ambayo hukubali mazao mbalimbali. |
No comments: