TWIGA STARS KUMENYANA NA TIMU YA WAANDISHI WA HABARI MKOANI MWANZA.
![]() |
Wanahabari Mkoani Mwanza wakinasa Habari kuhusiana na Mechi inayotarajiwa kuchwa Jumapili ijayo katika ya Twiga Stars na Timu ya Watangazaji na Wanahabari Mkoani Mwanza katika dimba la CCM Kirumba. |
Kona ya Michezo ya Kwa Neema Radio ya Jijini Mwanza, wameandaa Mchezo wa Soka kwa lengo la kutafuta pesa zinakazosaidia katika kupambana na ugonjwa huo.
Mchezo huo ambao utapigwa Jijini Mwanza jumapili
ijayo ya Octoba Tano katika Dimba la CCM Kirumba kuanzia majira ya saa 10
alasiri, utakuwa ni kati ya Timu ya Taifa ya Wanawake “Twiga Stars” dhidi ya
Mashujaa wa Kalamu na Sauti kwa maana ya Waandishi wa Habari na Watangazaji
Mkoani Mwanza.
Akizungumza na wanahabari Mkoani Mwanza Mkurugenzi
wa Born To Help Foundation ambaye pia ni mtangazaji wa kipindi cha kona ya
michezo katika kituo cha radio cha Kwa Neema Fm Erasto Juma alisema kuwa kutakuwa
mbali na mechi hiyo baina ya watangazaji na wanahabari Mkoani Mwanza dhidi ya
Twiga Stars pia kutakuwa na Mechi ya utangulizi
kati ya Geita Venterans dhidi ya Matajiri wa Alimas, Mwadui Fc kutoka Mkoani
Shinyanga, mechi ambayo itapigwa majira ya saa 8:00 za Mchana katika dimba hilo
hilo la CCM Kirumba.
Aidha Juma alisema kuwa asilimia kumi
ya mapato yatakayopatikana katika mchezo huo itapelekwa katika hospitali ya
Mkoa wa Mwanza Sekour Toure kwa aajili ya kuwasaidia wanawake wanaosumbuliwa na
saratani ya shingo ya kizazi huku akiongeza kuwa Kauli mbiu ya mchezo huo wa
kijamii itakuwa ni "Tuungane na kupiga vita Kansa ya Shingo ya kizazi. Nani
kama Mama”.
Kwa upande mwingine Juma alibainisha kuwa viingilio katika mechi hiyo vimepangwa kuwa ni sh.2,000 jukwaa la mzunguko na sh. 5,000 jukwaa kuu huku pia akiwataka wadau wadau, taasisi na makampuni mbalimbali kujitokeza kudhamini mchezo huo kwa kuwasiliana naye kwa namba ya simu 0767 200 986.
Kwa upande mwingine Juma alibainisha kuwa viingilio katika mechi hiyo vimepangwa kuwa ni sh.2,000 jukwaa la mzunguko na sh. 5,000 jukwaa kuu huku pia akiwataka wadau wadau, taasisi na makampuni mbalimbali kujitokeza kudhamini mchezo huo kwa kuwasiliana naye kwa namba ya simu 0767 200 986.
![]() |
Wanahabari Mkoani Mwanza wakinasa Habari kuhusiana na Mechi inayotarajiwa kuchwa Jumapili ijayo katika ya Twiga Stars na Timu ya Watangazaji na Wanahabari Mkoani Mwanza katika dimba la CCM Kirumba. |
No comments: