LIVE STREAM ADS

Header Ads

GALAWA AWATAKA WANAWAKE KUWASAIDIA WAUME ZAO KUFANYA BIASHARA.

Balozi wa Kampeni ya mwanamke na uchumi Linah Sanga (Mwenye Kinasa Sauti) akitoa burudani huku mkuu wa mkoa wa Tanga chiku galawa na mkurugenzi wa Angels Moment wakifurahia pamoja naye ukumbini Nivera jijini Tanga
Mkuu wa mkoa wa Tanga mheshimiwa Chiku Galawa amewataka wanawake Mkoani humo kuwasaidia wanaume katika kazi mbalimbali za ujasiriamali ili kuinua kipato cha kaya na familia zao.

Mheshimiwa Galawa alitoa rai hiyo
jana katika ukumbi wa Naivera katika hotuba kwa wanawake na wajasiriamali wa mkoa wa Tanga wakati wa ufunguzi wa semina za kampeni ya mwanamke na uchumi zilizoanza mjini hapa.

Alisema mkoa wa Tanga unao wanawake wachapa kazi na stadi wa kujishughulisha isipokuwa wanakwamishwa na waume zao ambao wengi hubaki vibarazani kwa kunywa kahawa na kucheza bao bila kujishughulisha.

“Tangu nimefika hapa Tanga imekuwa ikinishangaza sana kwa jinsi wanaume zenu wanavyopenda kubaki nyumbani na kushindwa kufanya biashara pamoja na ninyi wake zao,kila siku nashuhudia wanawake mkijishughulisha kwa kazi mbalimbali za kuwaletea kipato,sasa mtapata mafunzo ya jinsi ya kufanya biashara endelevu nawasihi nendeni na waume zenu kwenye biashara zenu,shirikianeni katika biashara na matokeo yake yatakuwa mazuri” amesema

Alisisitiza kuwa ni aibu kwa vijana wa kiume kila siku kuomba misaada maofisini wakati wangeweza kufanya kazi,jambo ambalo linachangiwa na akina mama kutopenda kuwatuma kazi watoto wao wa kiume matokeo yake wanapokuwa watu wazima wanakaa majumbani bila kujishughulisha kama ilivyo sasa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampeni ya Mwanamke na uchumi Mahada Erick alisema kampeni ya mwanamke na uchumi inalenga kuibua hisia chanya miongoni mwa wanawake juu ya maamuzi sahihi ya fursa za biashara na matumizi sahihi ya rasilimali fedha na akiba.

Alisisitiza kuwa “Manunuzi ya vitu vingi visivyo vya lazima yamefanya biashara za wanawake wengi kushindwa kukua na kushindwa kurejesha mikopo kutoka taasisi mbalimbali walikokopa kwa kushindwa kuwa na nidhamu katika matumizi na kukopa kwa kukosa malengo ya kibiashara, hivyo Kampeni ya mwanamke na uchumi inaleta mawazo mbadala ya kujenga uwezo wa mwanamke wa mkoa wa Tanga kwa kuangalia raslimali mpya kama ardhi na kujua hali za afya itakuwa ni ukombozi kwa akina mama wengi”

Jumla ya wanawake 400 wanatarajiwa kupata elimu juu ya kutambua fursa,afya bora na uchumi imara kwa mwanamke,usimamizi wa fedha na uwekaji akiba pamoja na mwanamke na rasrimali ardhi,ambapo kwa mkoa wa Tanga  imewezeshwa na NSSF,PPF,PSPF,GEPF,UTT,TBS,LEGAL NAIVERA,TANGA BEACH RESORT pamoja na SSRA.
Balozi wa Kampeni ya mwanamke na uchumi Linah Sanga (Mwenye Kinasa Sauti) akitoa burudani huku mkuu wa mkoa wa Tanga chiku galawa na mkurugenzi wa Angels Moment wakifurahia pamoja naye ukumbini Nivera jijini Tanga
Balozi wa Kampeni ya mwanamke na uchumi Linah Sanga akitoa burudani huku mkuu wa mkoa wa Tanga chiku galawa na mkurugenzi wa Angels Moment wakifurahia pamoja naye ukumbini Nivera jijini Tanga.
Burudani kutoka kwa Balozi wa Kampeni ya Wanawake na Uchumi Msanii Linah Sanga ikiendelea.
Wanawake wajasiriamali mkoani Tanga wakifurahia hotuba ya mkurugenzi wa Angels Moment Naima malima (Hayupo Pichani).
MKUU WA MKOA WA TANGA MHESHIMIWA CHIKU GALAWA akitoa hotuba ya ufunguzi wa kampeni ya mwanamke na uchumi jijini Tanga leo,katika ukumbi wa Naivera.
pix-6467 -Mkurugenzi wa kampeni ya mwanamke na uchumi Mahada Erick akitoa hotuba yake katika ufunguzi wa kampeni ya mwanamke na uchumi mkoani Tanga leo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Angels Moment Naima Malima akiwasilimia wanawake wa Mkoa wa Tanga[hawapo pichani] katika ufunguzi wa Kampeni ya Mwanamke na Uchumi Mkoani humo uliofanyika siku ya jana.
Mkurugenzi wa kampeni ya mwanamke na uchumi Mahada Erick akitoa hotuba yake katika ufunguzi wa kampeni ya mwanamke na uchumi Mkoani Tanga uliofanyika jana.
Balozi wa Kampeni ya mwanamke na uchumi Mwanamziki Linah Sanga.
Wanawake wajasiriamali kutoka wilaya mbalimbali mkoani Tanga wakifuatilia hotuba za mkuu wa mkoa wa Tanga[hayupo pichani] na ya mkurugenzi wa kampeni ya mwanamke na uchumi.
Na:Christian Gideon, Angels moment.

No comments:

Powered by Blogger.