WAKAZI WA MTAA WA IGOGO JIJINI MWANZA WAKUMBWA NA BOMOA BOMOA.
Mali mbalimbali za Wananchi wanaoishi Mtaa wa Igogo-Mrungushi Jijini Mwanza baada ya kutolewa nje kwa madai kuwa eneo wanapoishi wananchi hao ambao wengi wao ni wapangaji limeuzwa. |
leo wamepatwa na taharuki baada kuondoshwa katika nyumba walizokuwa wakiishi kwa amri ya mahakama kwa madai kwamba eneo hilo limeuzwa.
Wananchi hao ambao wengi wao walikuwa ni
wapangaji sanjari na wengine ambao walikuwa na shughuli zao za kibiashara
katika eneo hilo, wamekutwa na kadhia hiyo majira ya saa moja za asubuhi baada
ya mali zao kuondolewa katika nyumba walizokuwa wakiishi.
Habari kutoka eneo la tukio
zimeelezwa kuwa eneo zilipo nyumba walizokuwa wakiishi wananchi hao kama
wapangaji lilikuwa limeuzwa, lakini kutokana na wao kupata taarifa ya kuwataka kuhama
waliendelea kuishi katika nyumba hizo hadi hii leo walipovurumishwa na mali zao
kutolewa nje.
Kufuatia kadhia hiyo, wananchi hayo wameelezea kusikitishwa kwao
kutokana na hatua ya kuwahamisha katika eneo hilo kuchukuliwa huku wao wakiwa
hawana taarifa yoyote jambo ambalo wamesema kuwa limewasababishia hasara kubwa
kutokana na mali zao kuharibiwa vibaya wakati wa kuhamishwa huku nyingine
zikiibiwa mbaya zaidi wakiwa hawajui pa kwenda kutokana na jambo hilo kufanyika
ghafla.
Wakizungumzia tukio hilo, viongozi wa Kata ya Igogo wamesema kuwa
tukio hilo hata kama limetekelezwa kwa amri ya mahakama, halijazingatia haki na
sheria kwa kuwa wapangaji waliokuwa wakiishi katika nyumba hizo hawakupewa
taarifa ya kuwataka kuondoka katika nyumba hizo.
“Hata kama mmiliki wa eneo hili alipewa taarifa ya kumtaka kuondoka
katika hili eneo, bado taarifa zilipaswa kutolewa kwa wapangaji ikiwa ni pamoja
na kubandika taarifa hizo katika kuta za nyumba hizi ili wapangaji kuweza
kuchukua hatua ya kuhama mapema”.Alisema Maicco Maungo ambae ni Mwenyekiti wa
CCM Kata ya Igogo.
Baada ya tukio hilo la kuwaondoa wapangaji hao waliokuwa wakiishi
katika nyumba zilizokuwa katika eneo lililopo katika Mtaa wa Igogo-Mrungushi
Jijini Mwanza, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela Henry Matata ametoa kiasi
cha shilingi Laki tano kwa ajili ya kuwasaidia wapangaji waliokumbwa na kadhia
ya kuondolewa katika makazi waliyokuwa wakiishi.
Juhudi za kuwatafuta wahusika wa sakata hilo akiwemo Charles Malesa ambae ni mmiliki wa eneo hilo
ambalo lilikuwa na nyumba hizo hazikuweza kuzaa matunda baada ya kutoweka
ghafla katika eneo hilo kufuatia bomoa bomoa katika eneo hilo sanjari na mtu anaedaiwa kununua eneo hilo pia nae hakuweza kupatikana ili kupata ukweli zaidi juu ya sakata hilo.
Imeelezwa kuwa eneo hilo liliuzwa na aliekuwa mmiliki wake ambae ni
Charles Malesa lakini uuzwaji wa eneo hilo ulileta mgogoro wa muda mrefu baina
yake na mnunuaji ambae mpaka sasa amefahamika kwa jina moja la Shaa, hali
ambayo iliyopelekea suala hilo kutinga katika Mahakama Kuu kanda ya Mwanza
ambayo hatimae ilitoa amri ya kuwa mmiliki wake halali ni Shaa (Mnunuaji).
Wananchi ambayo mali zao zimetolewa katika nyumba walizokuwa wakiishi wakiwa katika hali ya taharuki kufuatia kuamliwa kuondoka katika nyumba hizo kwa madai kwamba eneo hilo limeuzwa na mmiliki wake. |
Shughuli za kuondoa mali zilizokuwa katika eneo hilo la Igogo-Mrungushi zikiwa zinaendelea. |
Shughuli za kuondoa mali zilizokuwa katika eneo hilo la Igogo-Mrungushi zikiwa zinaendelea. |
Mary Raimond ambae ni Mjumbe wa Serikali ya Mtaa (kushoto) akizungumza kuhusiana na sakata la wananchi waliondolewa katika eneo la Igogo-Mrungushi. |
No comments: