LIVE STREAM ADS

Header Ads

SUMATRA KUHAKIKISHA BANDARI ZOTE HAPA NCHINI ZINATOA HUDUMA KATIKA KIWANGO CHA KIMATAIFA.

Mamlaka ya usafiri na usafirishaji wa nchi kavu na majini nchini (SUMATRA) imesema,  itahikisha kuwa Bandari zilizopo nchini zinatoa huduma kwa kiwango cha kimataifa ili ziweze kushindana na bandari za nchi jirani ikiwa ni pamoja na kupewa leseni.

Akizungumza katika mkutano  wa wadau wa Sekta ya usafiri wa maji uliofanyika
Jijini Mwanza kuhusu utekelezaji wa kanuni za leseni za shughuli za bandari, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Gilliard Ngewe alieleza kuwa Sumatra kama mdhibiti, imepewa jukumu la kuwezesha bandari zinatoa  huduma bora na zenye ufanisi.

Ngewe alieleza katika kuboresha utendaji na usimamizi wa shughuli za bandari, serikali ilipitisha kanuni za leseni  zinazofahamika kama SUMATRA (Licencing of Port Terminal Operators) Regulations, 2011  ikiwa ni moja ya Nyenzo inayotumiwa na mamlaka hiyo ili kufikia malengo yaliyo kusudiwa.

“kuendelea kukua kwa biashara za kimataifa kunashinikiza bandari zetu zilizopo katika ukanda wa bahari na katika maziwa yetu kulenga kutoa huduma kwa viwngo vya juu.” alisema Ngewe.

Alisema tangu kuanzishwa kwa kanuni hizo mwaka 2011, utekelezaji wake ulikuwa haujaanza kutokana na mamlaka kuona umuhimu wa kutoa elimu kwanza ya kanuni kwa waendeshaji wa bandari, hali inayopelekea kupatikana kwa manufaa yaliyo kusudiwa katika uboreshaji wa  bandari.

Aliyataja manufaa hayo kuwa ni pamoja na  kudhibiti ulinzi wa nchi kwa kuhakikisha taratibu na sheria za nchi zinazingatiwa ipasavyo hususani udhibiti wa watu, meli na bidhaa zinozo ingia na kutoka nchini kupitia bandari hasa enzi hizi za kuongezeka kwa ughaidi na biashara haramu za madawa ya kulevya.

Zingine ni  kurahisisha utekelezaji wa sheria mbalimbali za nchi zinazosimamiwa na idara na taasisi nyingine za serikali katika maeneo hayo ikiwa ni pamoja na sheria ya  Forodha, kanuni za afya Bandarini ambazo zimelenga kudhibiti uambukizaji wa maradhi kutoka nchi moja hadi nyingine.

Ngewe aliongeza kuwa, kwa upande wa kanda ya ziwa, ziwa viktoria ni miongoni mwa maeneo yenye bandari nyingi zisizo rasmi(zisizo na leseni) kutokana na hali hiyo, ni vema kukawepo na usimamizi imara ili kupwepo na huduma bora na salama.

“sasa Sumatra imepanga kutekeleza kanuni hizi za leseni za shughuli za bandari katika kipindi hiki cha kuanzia mwaka huu wa fedha 2014/2015” alisema.

Mwisho.
Na:Prisica Japhes.

No comments:

Powered by Blogger.