LIVE STREAM ADS

Header Ads

MABINGWA WA MASHINDANO YA MITUMBWI YA BALIMI EXRA LAGER 2014 MKOANI MWANZA WAPATIKANA.

Washindi wa Mashindano ya Mitumbwi Mkoa wa Mwanza Upande wa Wanaume wakipokea zawadi (Pesa taslimu Shilingi Laki Tisa) baada ya kuibuka Washindi wa Kwanza.
Mashindano ya mbio za Mitumbwi katika ngazi ya Mkoa wa Mwanza jana yamefanyika na hivyo kuwapata washindi watakaouwakilisha Mkoa wa Mwanza katika Mashindano ya Mbio hizo za Mitumbwi katika ngazi ya Kanda ya Ziwa mwaka huu.


Mashindano hayo yalifanyika katika Mwambao wa
Mwaloni Kirumba Jijini Mwanza ambapo kwa upande wa Wanaume Mtumbwi kutoka Sengerema uliokuwa ukiongozwa na Costantin Lusalage uliibuka bingwa wa Mashindano hayo na hivyo kujinyakulia kitita cha shilingi Laki Tisa.

Nafasi ya pili wanaume ilinyakuliwa na Mtumbwi kutoka Misungwi uliokuwa ukiongozwa na Elisha Jacob na hivyo kujinyakulia Shilingi Laki Saba huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na Mtumbwi kutoka Luchelele Jijini Mwanza uliokuwa ukiongozwa na Emmanuel Masanyiwa na kujinyakulia shilingi Laki Tano na hivyo kukamilisha nafasi tatu za Mitumbwi itakayoiwakilisha Mwanza katika Fainali za Mashindano hayo ya Mitumwi Kanda ya Ziwa.

 Kwa upande wa wanawake Mtumbwi kutoka Misungwi uliokuwa ukiongozwa na Joyce Aron uliibuka nambari moja na kujinyakulia zawadi ya Shilingi Laki Saba huku Mtumbwi uliokuwa ukiongozwa na Tabu Daud kutoka pia Misungwi ukiibuka mshindi katika nafasi ya pili na kujinyakulia shilingi Laki Sita na hivyo kukamilisha nafasi mbili kwa upande wa wanawake katika fainali za Mashindano hayo Kanda ya Ziwa.

Katika mbio hizo za Mitumbwi mwaka huu, Ukerewe imepewa hadhi ya Kmkoa hivyo mbio za kuwatafuta washindi kutoka Ukerewe zitafanyika jumamosi ijayo ya Novemba 15 huko huko Ukerewe ambapo fainali za Mbio hizo za Mitumbwi Kanda ya Ziwa zinatarajiwa kufanyika Desemba Sita Mwaka huu katika Mwambao wa Mwaloni Jijini Mwanza.

Mabingwa wa Mashindano hayo upande wa wanaume walielezea kuwa mashindano hayo yalikuwa na ushindani mkali lakini kutokana na kujituma katika mazoezi wameweza kufanikiwa kuibuka mabingwa huku wakiongeza kuwa waandaji wa mashindano hayo wanapaswa kuongeza zawadi kwa washindi kwa lengo la kuwasaidia kujikimu kimaisha zaidi.
Washindi wa Kwanza (Mtumbwi kutoka Sengerema) upande wa wanaume katika Mashindano ya Mitumbwi Mkoani Mwanza wakiwa katika Picha ya Pamoja na Mgeni Rasmi.
Washindi wa Pili upande wa wanaume (Mtumbwi Kutokea Misungwi) wakipokea zawadi zao kiasi cha Shilingi Laki Saba.
Washindi wa Pili upande wa wanaume (Mtumbwi Kutokea Misungwi) wakiwa katika picha ya Pamoja na Mgeni Rasmi.
Washindi wa Tatu upande wa Wanaume (Mtumbwi kutoka Luchelele Jijini Mwanza) wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi.Walijishindia Shilingi Laki Tano.
Washindi wa Kwanza wa Mashindano ya Mitumbwi Mkoani Mwanza upande wa Wanawake (Mtumbwi kutoka Misungwi) wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi. Walijishindia shilingi Laki Saba taslim.
Washindi wa Kwanza wa Mashindano ya Mitumbwi Mkoani Mwanza upande wa Wanawake (Mtumbwi kutoka Misungwi) wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi. Walijishindia shilingi Laki Saba taslim.
Washindi wa Pili katika Mashindano ya Mitumbwi Mkoani Mwanza (Mtumbwi Kutoka Misungwi) wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni Rasmi.Walijishindia shilingi Laki Sita.
Mkuu wa Polisi Wilaya ya Ilemela (Katikati) tayari kwa kupuliza kipenga kwa ajili kuanza kwa mbio za Mitumbwi Mkoa wa Mwanza.
"Tunashuhudia jama wanavyopiga Makasia".
Malack Staki (Kushoto) ambae ni Meneja Mauzo na Usambazaji Kanda ya Ziwa kutoka TBL akiwa na Edith Debwa (Kulia) ambae ni Meneja wa Bia ya Balidi Extra Lager katika Mashindano ya Mitumbwi yaliyofanyika Jana Mkoani Mwanza katika Mwambao wa Mwaloni Kirumba.
Mkuu wa Polisi Wilaya ya Ilemela (Kulia) ambae alikuwa Mgeni Rasmi katika Mashindano ya Mitumbwi yaliyofanyika jana Mkoani Mwanza.
Edith Debwa (Kulia) ambae ni Meneja wa Bia ya Balidi Extra Lager akizungumza katika Mashindano ya Mitumbwi yaliyofanyika Jana Mkoani Mwanza katika Mwambao wa Mwaloni Kirumba.
Malack Staki (Kulia) ambae ni Meneja Mauzo na Usambazaji Kanda ya Ziwa kutoka TBL akizungumza katika Mashindano ya Mitumbwi yaliyofanyika jana Mkoani Mwanza.
Raulent Kebwa ambae ni Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wapiga Makasia Mkoa wa Mwanza.Kebwa ndie alikuwa pia Jaji nambari Moja katika Mashindano ya Mitumbwi yaliyofanyika jana Mwaloni Kirumba katika ngazi ya Mkoa wa Mwanza.
Mbio za kuwatafuta mabingwa wa Kupiga Makasia katika Mashindano ya Mitumbwi Mkoani Mwanza zikiwa zimeng'oa nanga katika Mwambao wa Mwaloni Kirumba siku ya jana.
Mtumbwi kutoka Sengerema ambao uliibuka nafasi ya Kwanza katika Mashindano ya Mitumbwi ngazi ya Mkoa wa Mwanza yaliyofanyika jana katika Mwambao wa Mwaloni Kirumba Mkoani Mwanza ukiwasili.
Mtumbwi kutoka Misungwi ambao ulishika nafasi pili katika Mashindano ya Mitumbwi Mkoani Mwanza ukiwasili katika fukwe za Mwaloni Kirumba Mkoani Mwanza.
Burudani pia ilikuwa ni sehemu ya kunogesha Mashindano hayo ya Mitumbwi yaliyofanyika jana katika Mwambao wa Mwaloni Kirumba Mkoani Mwanza.
Baadhi ya Wananzengo waliofika katika Mwambao wa Mwaloni ili kushuhudia Mashindano ya Mitumbwi mwaka huu 2014 katika ngazi ya Mkoa wa Mwanza.
Majina ya Washindi katika Mashindano ya Mitumbwi ya Balidi Extra Lager 2014 Mkoa wa Mwanza upande wa Wanaume.Nafasi ya 10 hadi ya tano washindi walijipatia Shilingi Laki mbili na Elfu Hamsini, Mshindi wa nne Laki nne, Mshindi wa tatu Laki Tano, Mshindi wa Pili Laki Saba na Mshindi wa Kwanza Laki Tisa.
Majina ya Washindi katika Mashindano ya Mitumbwi ya Balidi Extra Lager 2014 Mkoa wa Mwanza upande wa Wanawake.Nafasi ya 10 hadi ya tano washindi walijipatia Shilingi Laki mbili, Mshindi wa nne na wa tatu Laki Tano, Mshindi wa Pili Laki Sita na Mshindi wa Kwanza Laki Saba.
Na:George Binagi.

No comments:

Powered by Blogger.