MACHINGA WATAKIWA KUJIUNGA NA SHIUMATZ ILI KUNUFAIKA NA FURSA ZILIZOPO.
Wafanyabiashara wadogo maarufu kama Machinga Jijini Mwanza, wametakiwa kujiunga na Shirika la Umoja wa Machinga Tanzania (SHIUMATZ)
ili waweze kufaidika na huduma zinazopatikana katika shirika hilo.
Wito huo umetolewa
wiki iliyopita na Mwenyekiti wa umoja huo Mkoani Masanja Matondo wakati akizungumza na wanahabari Ofsini kwake ambapo alieleza kuwa moja ya faida ya kujiunga na Shiuma, ni pamoja na kuwa na kitambulisho kwa kila mfanyabiashara kitakachowasaidia katika shughuli zao.
wiki iliyopita na Mwenyekiti wa umoja huo Mkoani Masanja Matondo wakati akizungumza na wanahabari Ofsini kwake ambapo alieleza kuwa moja ya faida ya kujiunga na Shiuma, ni pamoja na kuwa na kitambulisho kwa kila mfanyabiashara kitakachowasaidia katika shughuli zao.
Matondo alieleza kuwa
huduma nyingine zinazopatikana katika shirika hilo, ni pamoja na kuwatafutia machinga maeneo ya kudumu ya kufanyia
biashara zao na kuwawezesha kupata mikopo kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali za
kifedha.
“tunashirikiana na taasisi
za kifedha kama Equity Benki, Tujitegemee Tanzania Limited na
Access Benki kwa kupitia
uongozi wa wamachinga ili waweze kupata mikopo ya kukuza na uendeleza biashara
zao”alisema Matondo.
Pia alieleza kuwa taasisi hizo hutoa mikopo kwa wafanyabiashara kwa
kuangalia kama mfanyabiashara ana leseni
ya biashara hivyo
kupitia Shiuma machinga ambao hawana leseni ya biashara wanaweza kupata mikopo
kwa kupitia katika uongozi huo.
Aidha alisema kuwa machinga hawaruhusiwi kufanya
biashara katika maeneo yaliyo zuiliwa na kwamba kwa kufanya hivyo ni dhahiri kuwa watakuwa wanavunja sheria ilizowekwa na halmashauri ya Jiji la
mwanza.
Hata hivyo Matondo aliwataka Machinga
Jijini Mwanza kutambua kuwa Shiuma ni chombo kinachowasimamia katika
shughuli zao, hivyo ni vyema wakapeleka kero zao mapema ili kutafutiwa
utatuzi kabla hakujatokea matatizo
mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusababisha vurugu katika maeneo yao ya biashara.
Na:Prisca Japhes.
No comments: