LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAENDESHA PIKIPIKI MKOANI MWANZA WAGOMEA ZOEZI LA UBADILISHAJI WA NAMBARI MPYA ZA PIKIPIKI.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza (Aliesimama) akitoa taarifa ya Umoja huo katika Mkutano Mkuu uliofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha VETA Mkoa wa Mwanza. Mkutano huo pia uliambatana na uchaguzi wa kuwachagua viongozi wa Umoja watakaoongoza katika kipindi cha miaka mitatu ijayo.
Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza umeweka msimamo mkali wa kutobadili nambari za pikipiki, kutokana na kile Umoja huo ulichokieleza kuwa ni zoezi hilo kufanyika huku waendesha pikipiki wakiwa hawajashirikishwa ipasavyo katika zoezi hilo la kubadili nambari za pikipiki.

Mwenyekiti wa Umoja huo
Makoye Kayanda alitoa kauli hiyo jana katika Mkutano Mkuu wa Umoja huo uliofanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi VETA Mkoani Mwanza, Mkutano ambao ulienda sambamba na Uchaguzi Mkuu wa kuwachagua Viongozi wa Umoja huo.

Makoye alibainisha kuwa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza unapinga vikali zoezi la kubadili nambari za pikipiki kutoka zinazotumika hivi sasa kwenda katika nambari mpya, kutokana na zoezi hilo kuanza kutekelezwa huku waendesha pikipiki wakiwa hawajashirikishwa ipasavyo kwa lengo la kujua dhana nzima ya kubadili namba hizo.

"Huu ni mradi ambao tayari Serikali imeuanzisha kwa ajili ya baadhi ya watu ili kujipatia kipato.Najua Serikali imetoa muda wa miezi sita hadi kufikia mwakani mwezi wa tatu pikipiki zote ziwe zinatumia nambari mpya, lakini sisi Mkoa wa Mwanza hilo suala tutalipinga na tutakwenda mahakamani ili kupinga suala hilo".Alisema Makoye wakati akizungumza mapema kabla ya uchaguzi ambapo hata hivyo alitetea kiti chake kwa kuchaguliwa tena kuwa Mwenyekiti Mpya wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza.

Akizungumza kwa niaba ya Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama barabara (RTO) Mkoa wa Mwanza, Koplo Frances Muganyizi ambae alikuwa Mgeni Rsmi akitokea kitengo cha Elimu Ofisi ya RTO Mkoa wa Mwanza aliahidi kufikisha masuala yote mhimu yaliyozungumzwa katika Mkutano huo wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza kwa ajili ya utekelezaji zaidi.

Katika Mkutano huo wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza, Makoye Kayanda alichaguliwa kwa awamu nyingine ya Miaka Mitatu kuwa Mwenyekiti kwa kupata kura 100 kati ya wajumbe 102 ambapo kura moja ilikuwa ya hapana huku moja nyingine ikiharibika ambapo Makamu Mwenyekiti aliechaguliwa ni Seif Kagoma ambae alipata kura 77.

Nafasi ya Katibu Mkuu ilienda kwa Abubakari Rubelwa ambae alitetea nafasi yake kwa kupata kura 98, huku Katibu Mkuu Msaidizi akiwa ni Dida Kinemo ambae alichaguliwa kwa kupata kura 99 kati ya Kura 102 za wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja huo.
Mwenyekiti wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza Makoye Kayanda akizungumza katika Mkutano wa Umoja huo uliofanyika jana katika Ukumbi wa Mikutano wa  Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi VETA Mkoani Mwanza. Mkutano huo pia uliambata na uchaguzi wa viongozi wa Umoja huo ambapo Makoye alitetea tena Kiti cha na hivyo ataungoza Umoja huo kwa kipindi cha Miaka mingine Mitatu ijayo.
Mgeni Rasmi Koplo Frances Muganyizi (Mwenye Kinasa Sauti) ambae yuko kitengo cha Elimu kutoka Ofisi ya Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani (RTO) Mkoa wa Mwanza akizungumza kwa niaba ya RTO Mkoa wa Mwanza katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza uliofanyika jana katika Ukumbi wa  Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi VETA Mkoani Mwanza.
Koplo Frances Muganyizi (Kulia) ambae yuko kitengo cha Elimu kutoka Ofisi ya Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Mwanza akifuatiwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza Makoye Kayanda (Katikati) na kushoto ni Abubakari Rubelwa ambae ni Katibu Mkuu wa Umoja huo.
Koplo Frances Muganyizi (Kushoto) ambae yuko kitengo cha Elimu kutoka Ofisi ya Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Mwanza akiwa na Maxmillian Kailangana (Kulia) ambae ni Kaimu Katibu Tawala Wilaya ya Nyamagana katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoani Mwanza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.Kailanga alikuwa ni Mmoja wa wasimamiz wa Uchaguzi wa Kuwapata viongozi wa Umoja huo katika Kipindi ncha Miaka Mitatu ijayo.
Bahati Musiba (Kulia) ambae ni Afisa Mfawidhi wa Sumatra Mkoa wa Mwanza akifuatiwa na Makamu Mkuu wa Chuo cha VETA Mwanza (Kushoto) katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza uliofanyika jana katika Ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha VETA Mwanza.
Abubakari Rubelwa ambae ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza (Kulia) akiwa na Bahati Musiba (Katikati) ambae ni Afisa Mfawidhi wa Sumatra Mkoa wa Mwanza akifuatiwa na Makamu Mkuu wa Chuo cha VETA Mwanza (Kushoto).
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Umoja huo uliofanyika jana katika Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi VETA Mkoani Mwanza.Mkutano huo pia uliambatana na uchaguzi wa Viongozi wa Umoja huo.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Umoja huo uliofanyika jana katika Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi VETA Mkoani Mwanza.Mkutano huo pia uliambatana na uchaguzi wa Viongozi wa Umoja huo.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Umoja huo uliofanyika jana katika  Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi VETA Mkoani Mwanza. Mkutano huo pia uliambatana na uchaguzi wa Viongozi wa Umoja huo.
Viongozi wa Vyama vya waendesha pikipiki walioalikwa kutoka Mikoa jirani katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza uliofanyika jana.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Umoja huo uliofanyika jana katika  Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi VETA Mkoani Mwanza. Mkutano huo pia uliambatana na uchaguzi wa Viongozi wa Umoja huo.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Umoja huo uliofanyika jana katika  Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi VETA Mkoani Mwanza. Mkutano huo pia uliambatana na uchaguzi wa Viongozi wa Umoja huo.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Umoja huo uliofanyika jana katika  Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi VETA Mkoani Mwanza. Mkutano huo pia uliambatana na uchaguzi wa Viongozi wa Umoja huo.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Umoja huo uliofanyika jana katika  Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi VETA Mkoani Mwanza. Mkutano huo pia uliambatana na uchaguzi wa Viongozi wa Umoja huo.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Umoja huo uliofanyika jana katika  Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi VETA Mkoani Mwanza. Mkutano huo pia uliambatana na uchaguzi wa Viongozi wa Umoja huo.
Miongoni mwa wafadhiri wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza ambao ni Wauzaji wa Pikipiki aina ya FEKON wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Umoja huo jana.
Maafisa Masoko kutoka Bank ya NMB wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza.
Winniel Mahumbuga (Mwenye Kinasa Sauti) ambae ni Afisa Masoko kutoka Bank ya NMB Tawi la Kenyatta Jijini Mwanza akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza uliofanyika jana katika Ukumbi wa Mikutano uliopo katika  Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi VETA Mkoani Mwanza.
Afisa Masoko kutoka Bank ya NMB Kanda ya Ziwa.
Maxmillian Kailangana (Katikati) ambae ni Kaimu Katibu Tawala Wilaya ya Nyamagana akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoani Mwanza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.Kailanga alikuwa ni Mmoja wa wasimamiz wa Uchaguzi wa Kuwapata viongozi wa Umoja huo katika Kipindi ncha Miaka Mitatu ijayo.
Msoma Shairi.
Jackob Paul (Kushoto) ambae ni Mwenyekiti Umoja wa Waendesha Pikipiki kutoka Shinyanga akitoa salamu zake katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Waendesha Pikipiki Mkoa wa Mwanza wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Umoja huo uliofanyika jana katika  Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi VETA Mkoani Mwanza. Mkutano huo pia uliambatana na uchaguzi wa Viongozi wa Umoja huo.
Huu ndio Usafiri wetu na ndiyo uliotufikisha katika Ukumbi wa Mikutano uliopo  Chuo cha Elimu ya Mafunzo ya Ufundi VETA Mkoani Mwanza.
Na:George Binagi.

No comments:

Powered by Blogger.