LIVE STREAM ADS

Header Ads

WATOTO WALIO CHINI YA UMRI WA MIAKA 18 KUPATIWA MATIBABU YA MACHO BURE MKOANI MWANZA.

Mlemavu wa Macho akitumia kompyuta.
Wazazi na Walezi Mkoani Mwanza wametakiwa kuwapeleka Watoto wao wenye Umri chini ya Miaka 18 kupima na kupatiwa bure huduma ya matibabu ya Macho ili kuepukana na tatizo la upofu.

Wito huo ulitolewa jana katika Hospitali ya Mkoa wa Mwanza Sekou Toure na
Mratibu wa Huduma ya Macho Mkoani Mwanza Dr.Elizabert Makamba katika zoezi la utoaji wa huduma ya macho bure kwa watoto waliochini ya Umri wa Miaka 18.

“Matibabu ya macho yanaweza kutibiwa haraka ikiwa kama muathirika atafikishwa mapema Hospitalini kwa ajili ya matibabu”. Alisema Dr.Makamba huku akiwasisitizia wazazi na walezi kuwafikisha watoto wao walio chini ya umri wa miaka 18 kwa ajili ya matibabu ya macho yaliyoanza kutolewa bure jana Novemba 10 hadi Novemba 22 mwaka huu katika Hospitali ya Mkoa wa Mwanza Sekou Toure.

Kwa upande wake Meneja wa Huduma ya Mikoba kutoka CCBRT Oscar James Tendeje alieleza kuwa Matibabu ya Mapema ya Macho husaidia kukuza shughuli za Maendeleo hivyo ni vyema wakazi wa Kanda ya Ziwa wakajitokeza kwa wingi katika huduma hiyo ya uchunguzi na utoaji wa matibabu ya macho bure inayotewa kwa watoto walio chini ya umri wa Miaka 18.

Kwa Upande wao baadhi ya Wazazi na Walezi waliowapeleka Watoto wao katika huduma hiyo kwa siku ya jana walitoa shukrani kwa Madaktari wanaohusika katika kufanikisha zoezi hilo ambapo nao waliwashauri wazazi na walezi wengine kujitokeza kwa wingi na kuwapeleka watoto wao ili kupatiwa huduma hiyo.

Jana Novemba 10 nchi mbalimbali duniani kote ziliungana pamoja katika kuadhimisha Siku ya Macho duniani ambapo katika Mkoa wa Mwanza, Maadhimisho hayo yalienda sambamba na zoezi la upimaji na utoaji wa matibabu ya bure kwa watoto walio chini ya Umri wa Miaka 18 katika Hospitali ya Mkoa wa Mwanza Seko Toure, zoezi ambalo litafikia tamati Novemba 22 Mwaka huu.
Na:Jacktan Msafiri.

No comments:

Powered by Blogger.