NYERERE AWATAKA WAGOMBEA URAIS KUELEZA WATAKAVYOMALIZA TATIZO LA DAWA ZA KULEVYA.
“Kama
Mwl.Nyerere angekuwa hai angewataka wagombea wa nafasi ya urais wanaoibuka
kila kukicha kwenye uchaguzi ujao mwakani, kutaja wazi kuwa wangewezaje kumaliza
tatizo la kukithiri kwa dawa za kulevya linalomaliza nguvu
kazi ya Taifa na kuongeza utofauti wa kipato katika jamii”.
Hayo
yalizungumzwa jana Jijini Mwanza na
mtoto wa Hayati Mwalimu Nyerere, Madaraka Nyerere
wakati alipokuwa akiongea na uongozi wa chama
cha waandishi wa habari wa kupiga
vita matumizi ya dawa za kulevya na uhalifu Tanzania (OJADACT).
Madaraka
aliwafunda viongozi wa chama hicho juu ya kuwa jasili wa kuiokoa jamii inayoelemewa
na mzigo wa uteja wa matumizi ya dawa za kulevya na usafirishaji kwa kuitaka OJADACT kuwauliza watangaza nia ya kugombea nafasi ya
urais katika uchaguzi ujao kuwa wataweza vipi kutokemeza tatizo la
dawa za kulevya nchini.
Madaraka
aliongeza kuwa suala la mmonyoko wa maadili
ndilo linaochangia katika suala zima la
jamii kujihusisha na dawa za kulevya, hivyo nguvu za pamoja zitahitajika katika kumaliza
tatizo hilo.
“Nakumbuka
Mwalimu Nyerere alikuwa akihimiza suala
la maadili kuanzia ndani ya familia yake hadi kwa Taifa ili jamii iweze kujiepusha
na momonyoko wa kimaadili, hivyo ni wazi tumuenzi kwa kuyarudia maadili mema ili
tumalize tatizo la dawa za kulevya” AlisemaMadaraka.
Naye Bwana
Cosmas Muhoja ambae ni rafiki wa karibu wa familia ya Nyerere alisema kuwa
tatizo la dawa za kulevya linatokana na baadhi ya watu
kuwa na tamaa ya kupata mali bila kujali
athari za kimaisha kwa watu wengine, jambo ambalo limekuwa likipelekea kukithiri
kwa biashara ya dawa za kulevya.
Naye
Mwenyekiti wa OJADACT Edwin Soko alisema kuwa kipaumbele chao kwa rais ajaye wa
watanzania ni uwezo wake katika kupambana na tatizo la dawa za kulevya kwani jamii imekuwa ikiangamia
kila kukicha na hakuna jitihada za kutosha zinazowekwa ikilinganishwa na ukubwa
wa tatizo lenyewe.
Aliongeza
kuwa OJADACT inakusudia kufanya mdahalo wa wazi kwa watangaza
nia ya kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi ujao ili waweze kujieleza ni
namna gani wataweza kumaliza tatizo la
dawa za kulevya hapa nchini, na majibu yao yatakuwa moja ya vigezo vya kupimwa na
wananchi kama kweli wanaweza kuwa viongozi shupavu wa kuliongoza Taifa hili.
Soko
alisema kuwa Marekani iliwahi kukumbwa na kukithiri kwa tatizo la dawa za kulevya
hali iliyopelekea kuwepo kwa ajenda maalumu kwa wagombea wa nafasi ya urais katika
Taifa hilo na hatimaye Richard Nickson alifanikiwa kuja na ajenda ambayo ilisaidia
kupunguza tatizo hilo nchini Marekani.
No comments: