LIVE STREAM ADS

Header Ads

MIDAHALO YA KUPANGA VIPAUMBELE VYA KUONGOZA MIJADALA YA KAMPENI ZA UCHAGUZI MKUU KUFANYIKA MKOANI MWANZA.

Rosemary Mwakitwange (Kushoto) ambae ni Mwenyekiti Mtendaji wa Taasisi ya Mafunzo ya Biashara na Mawasiliano Africa Mashariki EABMTI (East Africa Busness and Media Trainining Institute) akizungumza na Wanahabari juu ya Midahalo inayotarajiwa kufanyika Mkoani Mwanza. Katikati ni Fabian Fanuel kutoka Kwa Neema Radio na Kulia ni Filbert Kabago kutoka Passion Fm Mwanza.
Taasisi ya Mafunzo ya Biashara na Mawasiliano Africa Mashariki EABMTI (East Africa Busness and Media Trainining Institute) kwa Kushirikiana na Taasisi ya Twaweza, inatarajia kuendesha Midahalo Mkoani Mwanza ikiwa na lengo la Kuibua vipaumbele vya Kimkoa vitakavyosaidia katika kuongoza Mijadala ya Kampeni za Uchaguzi Mkuu hapa nchini.


Rosemary Mwakitwange ambae ni
Mwenyekiti Mtendaji wa Taasisi hiyo na Mwongoza Midahalo hiyo aliyasema hayo hii leo Jijini Mwanza, wakati akizungumza na Wanahabari juu ya Midahalo hiyo ambayo inatarajiwa kufanyika Mkoani Mwanza.

Mwakitwange alibainisha kwamba katika Mkoa wa Mwanza itafanyika Midahalo miwili ikiwa ni katika Wilaya ya Nyamagana pamoja na Ilemela ambapo katika Midahalo hiyo, wazungumzaji wakuu wanatarajiwa kuwa ni pamoja na Wakurugenzi, Mameya, Vyama vya Siasa vyenye Uwakilishi bungeni, Wabunge, Madiwani, Asasi za Kiraia sanjari na Chama cha Wafanyabiashara hapa nchini TCCIA.

Alisema katika Wilaya ya Nyamagana, Mdahalo utafanyika katika Ukumbi uliopo Gold Crest Hotel Ijumaa ya Wiki hii ambapo itakuwa ni February 06, 2015 ambapo katika Wilaya ya Ilemela Mdahalo utafanyika Jumamosi ya February 07, 2015.

Alisema lengo la Midahalo hiyo ni kutoa fursa kwa Wananchi, Serikali na Wawakilishi wa Wananchi kujadili kwa pamoja na kutambua changamoto zilizopo, ili kuepuka kuwa wasindikizaji katika mijadala mbalimbali ya Kitaifa ambayo inatarajiwa kufanyika kupitia kwenye vyombo vya habari katika kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu hapa nchini.

Katika kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Mwezi Octoba mwaka huu hapa nchini, Taasisi ya Mafunzo ya Biashara na Mawasiliano Africa Mashariki EABMTI (East Africa Busness and Media Trainining Institute)  kwa Kushirikiana na Taasisi ya Twaweza kimeandaa Midahalo ya TANZANIA TUNAYOITAKA ambayo itakuwa ikirushwa katika kituo cha Runinga cha ITV hivyo Midahalo inayofanyika hivi sasa Mikoani imelenga kuibua vipaumbele vitakavyoongoza Mijadala katika Vipindi vya Midahalo ya TANZANIA TUNAYOITAKA.
Rosemary Mwakitwange ambae ni Mwenyekiti Mtendaji wa Taasisi ya Mafunzo ya Biashara na Mawasiliano Africa Mashariki EABMTI (East Africa Busness and Media Trainining Institute).
Kushoto ni JeanPaul Fonkwa ambae ni Mwanasheria na Mshauri kutoka Taasisi ya Mafunzo ya Biashara na Mawasiliano Africa Mashariki EABMTI (East Africa Busness and Media Trainining Institute), ambapo Kulia ni Bi. Alawiya Mratibu kutoka EABMTI.
Baadhi ya Wanahabari kutoka Vyombo mbalimbali vya habari Mkoani Mwanza ambapo Kuushoto ni Filbert Kabako kutoka Passion Fm, Katikati ni Mr. Cathbert kutoka Afya Radio na Kulia ni Dotto Bulambu kutoka Radio Saut & Star Tv.
Wa kwanza Kushoto ni JeanPaul Fonkwa ambae ni Mwanasheria na Mshauri kutoka Taasisi ya Mafunzo ya Biashara na Mawasiliano Africa Mashariki EABMTI (East Africa Busness and Media Trainining Institute). Wa tatu kutoka Kushoto ni Simba Ulanga Kutoka City Fm-Mwanza na Wa kwanza Kulia ni Neema Joseph kutoka Gazeti la Zanzibar leo.
Taswira ya Kikao kifupi katika ya Wanahabari Mkoani Mwanza na  baadhi ya Viongozi kutoka Taasisi ya Mafunzo ya Biashara na Mawasiliano Africa Mashariki EABMTI (East Africa Busness and Media Trainining Institute) ilivyokuwa, ambapo Kikao hicho kimefanyikia Vizano Hotel Mapema hii leo.
Na: George Binagi-GB Pazzo.

No comments:

Powered by Blogger.