Viongozi mbalimbali wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mkoa wa Mwanza wakiwa katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika hii leo katika Tawi la Ziwa lililopo Kata ya Butimba, Wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza ambapo aliekuwa Mfuasi na Kiongozi katika nafasi mbalimbali ndani ya Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mwanza Veronica Method Tuhoye (Mwenye saa Mkononi) amehamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema. Miongoni Mwa nafasi alizokuwa nazo Veronica Method Tuhoye ndani ya Chama cha Mapinduzi hadi anatimkia CHADEMA ni pamoja na Mjumbe Kamati Kuu CCM Wilaya ya Nyamagana, Mjumbe wa UWT ndani ya Mkutano Mkuu Mkoa wa Mwanza, Mjumbe baraza la Wanawake Wilaya ya Nyamagana pamoja na Mjumbe Kamati ya Siasa Kata ya Butimba Wilayani Nyamagana. Akipokea jana Kadi ya Chadema Tuhoye alisema kuwa ameondoka CCM na Kujiunga na CHADEMA kwa ajili ya kuwatumikia wananchi baada ya kuona kwamba ndani ya CCM hapati nafasi ya kufanya hivyo. |
No comments: