LIVE STREAM ADS

Header Ads

WANANCHI WILAYANI ILEMELA MKOA WA MWANZA WALIA NA ILEMELA WANAYOITAKA.

Wananchi Wilayani Ilemela Mkoani Mwanza wameilalamikia Ilemela walioyonayo hivi sasa kutokana na kuwa katika hali mbaya Kimaendeleo, ambapo wamebainisha kuwa wakati umefika wa Kuwa na Ilemela yenye Maendeleo.

Wameyasema hao jumamosi iliyopita katika Mdahalo wa Tanzania Tuitakayo ulioratibiwa na Taasisi ya Mafunzo ya Biashara na Mawasiliano Africa Mashariki EABMTI (East Africa Busness and Media Trainining Institute) kwa Kushirikiana na Taasisi ya Twaweza uliokuwa na lengo la Kuibua vipaumbele vya Kimkoa vitakavyosaidia katika kuongoza Mijadala ya Kampeni za Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika hapa nchini mwaka huu.
Wananchi hao walisema kuwa wangependa kuiona Ilemela yenye vipaumbele kadhaa vya kimaendeleo ambavyo ni pamoja na upatikanaji wa elimu bora ambapo katika suala la elimu walisema kuwa bado kuna idadi kubwa ya watoto ambao hawajapata fursa ya kuandikishwa kuanza masomo yao sanjari na kuwa na wananchi wengi wasiojua kusoma na kuandika.

Pia walieleza kuwa sehemu kubwa ya wilaya ya Ilemela bado ni vijiji kulinganisha na Wilaya jirani ya Nyamagana huku ikiwa inakabiriwa na ubovu wa miundominu ambayo walisema kuwa ni mibovu kuliko Wilaya yoyote ile hapa nchini huku wakiongeza kuwa bado Ilemela ina siasa chachu ambazo ni za chuki na zinapaswa kutokomezwa.

Aidha walisema kuwa kuwa Wilaya ya Ilemela bado iko ICU (iko katika hali mbaya) katika suala la huduma za Afya ambapo walilalamikia uhaba wa vituo vya Afya na Zahanati katika Kata nyingi za Wilaya ya Ilemela sanjari na Ukosefu wa Hospitali ya Wilaya huku wakishangazwa na kuwepo kwa Mganga Mkuu wa Wilaya ambae walihoji juu ya uwepo wake.

Ili kuipata Ilemela na Mwanza wanayoitaka Wananchi hayo walipendekeza wananchi kuchukua hatua kwa kubadili mfumo wa Uongozi walionao na kuwachagua viongozi ambayo watashirikiana na wananchi katika kuibadili sura ya Ilemela na hatimae kuwa na Ilemela Waitakayo yenye maendeleo.
Akizungumza katika Mdahalo huo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, Viola Mbalikle aliahidi kuyafikisha kwa Mkurugenzi wa Manispaa hiyo yale yote yaliyozungumza na wananchi kwa lengo la kufanyiwa kazi.

Katika Mkoa wa Mwanza ilifanyika Midahalo miwili ambapo katika Wilaya ya Nyamagana, Mdahalo ulifanyika katika Ukumbi uliopo Gold Crest Hotel siku ya Ijumaa ya wiki iliyopita ambapo ilikuwa ni February 06, 2015 na katika Wilaya ya Ilemela Mdahalo ulifanyika Jumamosi ya February 07, 2015.


Rosemary Mwakitwange ambae ni Mwenyekiti Mtendaji wa Taasisi hiyo na Mwongoza Midahalo hiyo alisema kuwa lengo la Midahalo hiyo ni kutoa fursa kwa Wananchi, Serikali na Wawakilishi wa Wananchi kujadili kwa pamoja na kutambua changamoto zilizopo, ili kuepuka kuwa wasindikizaji katika mijadala mbalimbali ya Kitaifa ambayo inatarajiwa kufanyika hivi karibuni ikiwa ni katika kuelekea kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu hapa nchini.
Na:George Binagi-GB Pazzo

No comments:

Powered by Blogger.