LIVE STREAM ADS

Header Ads

KATIBU WA CCM MKOA WA MWANZA AMTAKA MKUU WA WILAYA YA SENGEREMA KUSHUGHULIKIA MIGOGORO YA ARDHI WILAYANI HUMO.

Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Miraji Mtatuturu akiwasili hii leo katika Ofisi za Chama hicho Wilaya ya Sengerema kwa ajili ya Ziara ya Siku mbili Wilayani humo.
 Na:George Binagi-GB Pazzo
Chama cha Mapinduzi Mkoani Mwanza kimemtaka Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Zainabu Telaki kushughulikia matatizo ya ardhi, yanayowakabili wananchi wa Kijiji cha Mnadani Wilayani humo.

Katibu wa Chama hicho Mkoa wa Mwanza Miraji Mtatutu ametoa kauli hiyo hii leo katika Viwanja vya CCM Wilayani Sengerema, wakati akiwahutubia wananchi katika Mkutano wa hadhara.

Kauli ya Mtaturu imejili kufuatia malalamiko kutoka kwa Wananchi wa Kijiji hicho, kuwalalamikia maafisa wa ardhi Wilayani Sengerema kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa Kijiji cha Mnadani kuingia katika Mashamba yao kwa ajili ya upimaji wa ardhi bila kushirikishwa.

Mtaturu amebainisha kuwa sheria ya ardhi inaeleza wazi kuwa wananchi wanapaswa kushirikishwa kwanza katika uendelezaji wa ardhi yao, hivyo kitendo cha wananchi hao kutoshirikishwa katika upimaji wa ardhi yao ni uvunjifu wa sheria.

"Sheria ya ardhi iko wazi, kabla serikali haijaja kufanya chochote kwenye eneo lako lazima ikushirikishe...ukiona mtu anakuja kwako bila kukushirikisha mtoe nduki...wananchi hawa msiwaonee...Mkuu wa Wilaya shughulika na hii kitu...sisi shida yetu CCM wananchi matatizo yao yaishe" Amesema Mtaturu.

Awali akitoa malalamiko yake kwa niaba ya Wananchi wengine, Imelda Mpanduji ambae ni mwananchi wa Kitongoji cha Mnadani Wilayani Sengerema, amesema kuwa wananchi wamechoka kuburuzwa na viongozi hao ambao wamekuwa wakiingia katika mashamba yao na kupima ardhiri kinyemela na hivyo kumuomba katibu huo wa CCM Mkoa wa Mwanza kuingilia kati suala hilo kwa ajili ya kulipatia ufumbuzi.

Akijibu Malalamiko ya Wananchi hao, Staimili Alexander Ndaro ambae ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema ameeleza kuwa viwanja vinavyolalamikiwa na wananchi hao ni vile vinavyopitiwa na mradi wa kuendeleza Makazi ya wananchi katika eneo hilo la Mnadani Wilayani Sengerema, hivyo kama kuna mwananchi ambae amekosa kiwanja katika eneo hilo na ardhi yake imechukuliwa kwa ajili ya matumizi mengine ya Umma, anapaswa kufika katika Ofisi za Halmashauri hiyo kwa ajili ya kupatiwa kiwanja kingine.

Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu ameanza ziara yake ya siku mbili Wilayani Sengerema hii leo ikiwa ni mwendelezo wa ziara zake katika Wilaya za Mkoa wa Mwanza ambapo pamoja na mambo mengine amekutana na Kamati ya Siasa, Halmashauri kuu ya CCM ya Wilaya pamoja na kuzungumza na Wananchi katika Mkutano wa hadhara.


Akiwa katika kikao cha Halmashauri kuu ya CCM ya Wilaya ya Sengerema Mtaturu amewataka wanachama wa chama wa chama hicho kuwa wamoja na kuachana na mgawanyiko ndani ya chama ambapo ametahadharisha kuwa CCM bado iko imara na itaendelea kutawala milele na milele.

Kesho ziara hiyo inatarajiwa kuhitimishwa ambapo Mtaturu anatarajia kukagua shughuli za miradi ya maendeleo ambazo ni pamoja na kukagua miradi ya maji Luchili, Lumeya, Nyakaliro lakini pia kukagua Maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya Isaka Nyehunge na hatimae kutamatisha ziara hiyo kwa kufanya Mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Nyakaliro Jimboni Buchosa.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu (Aliesimama) akizungumza na Halmashauri ya CCM Wilaya ya Sengerema hii leo.
Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Zainabu Telaki (aliesimama) akiwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Serikali ya Mwaka 2010/15 katika kikao cha halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Sengerema kilichofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Sengerema.
Wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Sengerema wakiwa katika kikao na Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu (Alie Jukwaani) akiwahutubiwa wananchi Wilayani Sengerema katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya CCM Wilayani humo.
Wananchi na Wanachama wa CCM wakimsikiliza Katibu wa ccm Mkoa wa Mwanza.
Watendaji pamoja na Viongozi wa CCM na Serikali Wilayani Sengerema.
Watendaji pamoja na Viongozi wa CCM na Serikali Wilayani Sengerema.
Akijibu Malalamiko ya Wananchi hao, Staimili Alexander Ndaro ambae ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema akijibu malalamiko ya Wananchi kuhusiana na upimaji wa ardhi yao bila kushirikishwa.
SOURCE:99.4 METRO FM

No comments:

Powered by Blogger.