LIVE STREAM ADS

Header Ads

SHIRIKISHO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI KANDA YA ZIWA LAZINDULIWA KWA STYLE YA PEKEE.

Na: George Binagi-GB Pazzo
Shirikisho la Waimbaji wa Muziki wa Injili Kanda ya Ziwa, limezinduliwa Rasmi katika Uwanja wa CCM Kirumba Ilemela Mkoani Mwanza, ambapo uzinduzi huo uliambatana na Tamasha kubwa la Marafiki.

Akizungumza jana katika Uzinduzi wa Shirikisho hilo, Idd Juma ambae ni Mratibu wa Tamasha la Marafiki lililoambatana na Uzinduzi huo alisema kuwa lengo la kuanzisha Shirikisho la Waimbaji wa Muziki wa Injili Kanda ya Ziwa ni kuuinua muziki huo sanjari na waimbaji wake hususani katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa na Tanzania kwa ujumla.

Alibainisha kwamba ndani ya Shrikisho hilo kutakuwa na Muungano wa Vyama mbalimbali ambavyo ni Chama cha Wanakwaya, Chama cha Band za Injili, Chama cha Waimbaji binafsi, Chama cha Watangazaji wa muziki wa Injili wa radio na Tv, Chama cha Waalimu wa Kwaya, Chama cha wapiga Muziki wa Injili pamoja na Chama cha Watengenezaji wa Muziki wa Injili.

Kwa pamoja Juma alisema kuwa vyama hivyo ndivyo vinavyounda Shirikisho la Waimbaji wa Muziki wa Injili Kanda ya Ziwa, huku akiongeza kuwa ili Muziki wa Injili uweze kupiga hatua zaidi, Shirikisho hilo limeadhimia kuanzisha Studio kwa ajili ya kuwasaidia waimbaji wa Muziki wa Injili kurekodi kazi zao kwa gharama nafuu.

Aidha Juma alitoa rai kwa Watanzania kuipigania na kuendelea kuienzi amani ya Tanzania huku akikemea vitendo vya Utekaji na Mauaji ya Watu wenye Ulemavu wa ngozi ambavyo vimeonekana kushamiri hapa nchini hususani katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Mgeni Rasmi katika Tamasha hilo la Marafiki Dede Petro ambae ni Mwenyekiti wa Chama cha Madereva wa Daladala Kanda ya Ziwa, alitoa rai kwa waimbaji wa Muziki wa Injili ya Ziwa kuendelea kushikamana kwa pamoja ambapo pamoja na mambo mengine alichangia Shilingi Laki Tano kwa ajili ya kusaidia Shirikisho hilo la Waimbaji wa Muziki wa Injili Kanda ya Ziwa.

Wakishiriki katika kuchangia harambee ya kuimarisha Shirikisho hilo la Waimbaji wa Muziki wa Injili, Dede Swila Dede ambae ni Diwani wa Kata ya Mgogwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela pamoja na Sarah Paul Ng’wani ambae ni diwani Viti Maalumu katika Manispaa hiyo, waliwasihi Watanzania kuhakikisha kwamba wanailinda Amani ya Tanzania hususani katika kipindi hiki cha kuelekea katika Uchaguzi Mkuu ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba utekaji na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi yanatokomezwa mara moja.
Idd Juma ambae ni Mratibu wa Tamasha la Marafiki lililofanyika jana katika Uwanja wa CCM Kirumba Ilemela Mkoani Mwanza.
Mgeni Rasmi katika Tamasha hilo la Marafiki Dede Petro ambae ni Mwenyekiti wa Chama cha Madereva wa Daladala Kanda ya Ziwa (Kulia). Kushoto ni Joel Maduka mwanahabari kutoka Kwa Neema Radio Mkoani Mwanza.
Mgeni Rasmi katika Tamasha hilo la Marafiki Dede Petro ambae ni Mwenyekiti wa Chama cha Madereva wa Daladala Kanda ya Ziwa (Kulia). Kushoto ni Joel Maduka mwanahabari kutoka Kwa Neema Radio Mkoani Mwanza.
Dede Swila Dede ambae ni Diwani wa Kata ya Mgogwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza. 
Sarah Paul Ng’wani ambae ni diwani Viti Maalumu katika Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza.
Joseph Boniface (wa kwanza kulia) ambae ni Marketing Manager Kampuni ya Proin Promotion Mwanza.

No comments:

Powered by Blogger.