LIVE STREAM ADS

Header Ads

WATU WATANO WAANGUKIWA NA UKUTA KATIKA ENEO LA UJENZI JIJINI MWANZA.

Mapema hii leo wakati wa zoezi la kuwaokoa watu waliodondokewa na Ukuta wakati wakiwa katika shughuli ya Ujenzi Jijini Mwanza.
Na:Prisca Mshumbuzi
Watu watano wamenusirika kifo baada ya kudondokewa na ukuta ambao ujenzi wake ulikuwa ukiendelea kujengwa katika eneo la kitalu namba sita, block U barabara ya Nyerere Jijini Mwanza.

Akizungumza muda mfupi baada ya tukio hilo, msimamizi wa ujenzi huo Williamu Issa alisema kuwa watu hao ambao ni mafundi walikumbwa na tukio hilo hii leo majira ya saa tano asubuhi, wakati wanafukia sehemu ya ardhi ambayo kulikuwa na mmomonyoko wa udongo na ndipo ghafla ukuta ukawadondokea.

Muuguzi wa zamu kitengo cha wagonjwa wa dharula hospitali ya rufaa bugando, Dk. Ernest Elisenguo alithibitisha kupokea majeruhi hao ambapo majeruhi wawili walikuwa katika hali mbaya huku majeruhi akifafanua kuwa hali za majeruhi watatu hazikuwa mbaya sana hivyo watatibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani.

Aliwataja wagonjwa  ambao hali yao haikuwa nzuri kuwa ni Benson Daudi ambaye hali yake ilikuwa mbaya kiasi cha kupoteza fahamu kutokana na kupata mtikisiko kichwani, Rashidi Mkumba ambaye amevunjika mguu wa kushoto pamoja na mbavu.

Dr.Elisengue aliwataja majeruhi  watakao ruhusiwa kurudi nyumbani baada ya matibabu kuwa ni Elias Bahati, Agustino Msindi na Ramadhani Nyarandu ambao hali yao ilionekana kuimarika wakati wakiendelea kupata huduma.


Naye Mkuu wa wilaya ya Nyamagana  Baraka Konisa aliagiza ujenzi huo usimame hadi pale uchunguzi utakapo kamilika ili kuweza kubaini chanzo kamili cha kuanguka kwa ukuta huo.
Mapema hii leo wakati wa zoezi la kuwaokoa watu waliodondokewa na Ukuta wakati wakiwa katika shughuli ya Ujenzi Jijini Mwanza.
SOURCE:BINAGI MEDIA GROUP

No comments:

Powered by Blogger.