LIVE STREAM ADS

Header Ads

ZITTO KABWE AVULIWA RASMI UANACHAMA NDANI YA CHADEMA.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe amevuliwa rasmi uanachama ndani ya Chama Cha Demokrasia na maendeleo (Chadema), baada ya Mahakama Kuu Tanzania kanda ya Dar es Salaam leo kutupilia mbali kesi aliyokuwa ameifungua dhidi ya chadema akihoji uhalali wa uanachama wake ndani ya chama hicho.

Habari zinaeleza kuwa Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na maendeleo Tundu Lissu ametangaza kuvuliwa rasmi uanachama wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe.
Akitangaza mapema leo hatua hiyo ya kumvua uanachama, Lissu alisema kanuni na sharia za chama hicho ziko wazi na zinaelekeza kuwa endapo mwanachama yeyote atakishtaki chama hicho mahakamani na iwapo atashindwa atakuwa amejiondoa mwenyewe kwenye chama.
"Kwa mujibu wa katiba ya chama cha CHADEMA, mwanachama yoyote anapofungua kesi mahakamani dhidi ya chama chake, endapo atashindwa katika kesi hiyo atakuwa amejiondoa uanachama wake, kwa hiyo natangaza rasmi rasmi Zitto Kabwe sio mwanachama tena wa Chadema” Alisema Lissu.
Mbali na hayo Mahakama Kuu Kanda ya Dar es salaam imeamuru CHADEMA kulipwa gharama zote za kuendeshea case hiyo hiyo ikiwa na maana kwamba Zitto anapaswa kulipa gharama zote za kesi hiyo na kwamba hakuna shauri lolote Mahakamani kwa sasa.


Mwaka jana Zitto Kabwe aliweka pingamizi mahakamni kuzuia kikao cha Kamati Kuu kumjadili ambapo hoja yake ilikuwa kupinga kuitisha kamati kuu kabla shauri lake halijasikilizwa na Baraza Kuu ambapo alitaka mahakama iagize kamati kuu ya CHADEMA kutojadili suala lake mpaka baraza kuu likae kuamua rufaa yake.
NA MHARIRI: BINAGI MEDIA GROUP KWA MSAADA WA MTANDAO.

No comments:

Powered by Blogger.