LIVE STREAM ADS

Header Ads

KATIBU WA CCM MKOA WA MWANZA ATOA AGIZO KWA MANISPAA YA ILEMELA.

Na:George GB Pazzo
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza imetakiwa kurekebisha daraja la Msuka lililopo Kilimahewa, linaunganisha barabara ya Isanga Kiloleni ili kuondoa adha wanayoipata watumiaji wa barabara hiyo wakati wa Mvua.

Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoani Mwanza Miraji Mtaturu alitoa kauli hiyo jana alipofanya ziara ya kutembelea daraja hilo, wakati wa ziara yake ya kukagua Miradi ya Maendeleo Wilayani Ilemela.

Wakati wa mvua daraja hilo huwa halipitiki kutokana na maji kujaa na kupita juu yake, na hivyo kuzagaa ovyo hadi katika nyumba na makazi ya wananchi.

Katika hatua nyingine, Mtaturu alitoa muda wa mwezi mmoja kwa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela iwe imejenga daraja la Ujiji linalopitisha Maji ya Mto Msuka liwe limejengwa baada ya kubomolewa na Maji ya Mvua zinazoendelea kunyesha Mkoani Mwanza na hivyo kuhatarisha maisha ya watumiaji wake hususani wanafunzi wa shule za msingi.


Kwa Upande wa Daraja la Msuka, Mhandisi wa Barabara kutoka Manispaa ya ilemela Mikidadi Adam alisema kuwa Manispaa hiyo iko katika hatua za mwisho za kumpata Mkandarasi kwa ajili ya kurekebisha changamoto za Miundombinu zilizopo katika Manispaa hiyo, hivyo ndani ya miezi mitatu miundombinu yote katika Manispaa hiyo likiwemo daraja la Msuka itakuweza kurekebishwa.
                               BONYEZA HAPA KUJIONEA ZAIDI

No comments:

Powered by Blogger.