MKATABA WA NGASSA KWISHA SASA ANAPIGA DEIWAKA YANGA.
Na:Genya Richard
Imebainika kwamba Kuanzia jana April 20 Mrisho Ngassasi ambae ni mchezaji wa Timu ya Soka ya Yanga Sport Club, anapiga deiwaka (anaitumikia Yanga bila Mkataba) katika Klabu hiyo kufuatia kumalizika kwa mkataba wake.
Imebainika kwamba Kuanzia jana April 20 Mrisho Ngassasi ambae ni mchezaji wa Timu ya Soka ya Yanga Sport Club, anapiga deiwaka (anaitumikia Yanga bila Mkataba) katika Klabu hiyo kufuatia kumalizika kwa mkataba wake.
Hata hivyo kwa mjibu wa kanuni za soka Ngassa
ataendelea kuichezea timu hiyo hadi kumalizika msimu huu kwa kuwa amesajiliwa
kuichezea Yanga katika mashindano yote ya ndani na nje ya nchi.
Binagi Media Group kitengo cha Michezo jana April
20 kiliarifiwa kuwa Ngassa alimaliza mkataba
wake wa miaka miwili na Yanga na hajasini mkataba mpya.
“Kwa sasa sitaki kuzungumzaia masuala ya mkataba,
nataka nimalize msimu kabisa ndiyo nianze mjadala wa mkataba mpya. Mimi ni
mchezaji niliyesajiliwa Yanga msimu huu hivyo baada ya msimu kuisha ndipo mambo
mengine yatafuata”. Alisema Ngassa wakati akizungumza na Binagi Media Group.
Kuhusu uvumi kuwavamesaini timu ya Free State
ya Afrika kusaini, Ngassa alisema “Nipo kwenye mazungumzo na timu tatu ikiwemo hiyo ya Free State na nyingine
ya Qatar na pia nimeletewa ujumbe kwamba As Vita ya Congo na Etoile ya Tunisia nao
wananifuatilia. Lakini mimi sina papara kwani nasubiri nimalize msimu wangu
kwanza” Alisema Ngassa huku akisisitiza kuwa atakuwa tayari kuzungumzia masuala
ya mkataba mpya baada kumalizika kwa msimu wa Soka wa Mwaka 2014/15.
BINAGI MEDIA GROUP PRODUCTION
No comments: