BASI LA BUNDA EXPRESS LAPINDUKA JIJINI MWANZA.
Picha kutoka Maktaba
ELISA ANATORY/ 0763345064
EMAIL anatoryelisa@gmail.com
Watu wanne wamejeruhiwa katika ajali ya basi
iliyotokea jana katika eneo la Tanesco barabara ya Kenyatta Jijini Mwanza.
Ajali hiyo ilitokea majira ya saa kumi na moja za alfajiri ikihusisha basi la Bunda express
lenye namba za usajili T 318 CXZ linalofanya safari za Mwanza kwenda Bukoba Mkoani Kagera ambapo lilikuwa likitokea Kituo Cha Mabasi Buzuruga
kuelekea Kituo cha Mabasi Nyegezi ambapo.
Chanzo cha ajali hiyo ni
baada ya dereva kushindwa kukwepa gari la kushindilia barabara lililokuwa
limepaki katika Barabara Kenyata eneo la
eneo la Tanesco ambapo kuna matengenezo ya barabara.
Dakitari wa zamu wa hospitali ya Rufaa ya Bugando ambapo
majeruhi hao walipelekwa Edwini Mbwambo aliwataja majerui hao kuwa ni Alfan
Yusufu (50),Christian Iyakugilwa (65), Richard Malema (30) pamoja Valentine
Kalamagangara (30)
Baadhi ya Mashuhuda wa ajali
hiyo walieleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi ambapo dereva wa basi
hilo alishindwa kulimudu na hatimae kugonga gari la kushindilia barabara na
hatimae kupinduka.
Hadi tunakwenda mitamboni, Kamanda
wa Polisi Mkoani Mwanza alikuwa hajapatikana ili kuthibitisha kutokea kwa ajali
hiyo.
No comments: