LIVE STREAM ADS

Header Ads

KATIBU WA BAWACHA KATA YA BUTIMBA JIJINI MWANZA AWASHAURI WANAWAKE NCHINI.

Veronica Method Tuhuye ambae ni Katibu Mwenezi BAWACHA Kata ya Butimba Jijini Mwanza
Na:Binagi Media Group
Wanawake nchini wameshauriwa kushiriki katika Shughuli mbalimbali za Kimaendeleo zinazowazunguka na hivyo kuachana na misingi ya Kubweteka kutokana na Mazoea na dhana ya Kusubiri kuwezeshwa.

Rai hiyo ilitolewa jana na Veronica Method Tuhuye ambae ni Katibu Mwenezi wa Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA (BAWACHA) Kata ya Butimba Jijini Mwanza, wakati akizungumzia nafasi ya Mwanamke ndani ya Chadema katika kuwania nafasi mbalimbali za Uongozi.

Tuhuye alisema kuwa ndani ya Chadema wanawake wanapata fursa mbalimbali za Kuwania nafasi za Uongozi ambapo jambo kubwa lililopo ni wanawake wenyewe kujiamini na kujitokeza kwa wingi katika kuwania nafasi hizo.

Aidha Tuhuye aliwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi katika Mkutano wa Hadhara unaotarajiwa kufanyika Wiki hii katika Kata yake ya Butimba, Mkutano ambao utafanyika siku ya  Alhamisi ya May 21 katika Uwanja Butimba Sokoni ambapo mzungumzaji Mkuu anatarajiwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Ezekiel Wenje (Chadema).

Katika hatua nyingine Tuhuye ambae alijiunga na Chadema tangu Mwezi Januari mwaka huu akitokea CCM, alibainisha kuwa ndani ya Chadema kuna jukumu moja tu la kuwatumikia Watanzania bila kujali kujuana tofauti na CCM ambapo hali ni tofauti na kwamba nafasi za uongozi zinatolewa kwa kujuana.
BONYEZA PLAY HAPA CHINI KUSIKILIZA
Veronica Method Tuhuye ambae ni Katibu Mwenezi BAWACHA Kata ya Butimba Jijini Mwanza
Veronica Method Tuhuye ambae ni Katibu Mwenezi BAWACHA Kata ya Butimba Jijini Mwanza
Veronica Method Tuhuye ambae ni Katibu Mwenezi BAWACHA Kata ya Butimba Jijini Mwanza akizungumza nasi.

No comments:

Powered by Blogger.