LIVE STREAM ADS

Header Ads

KATIBU WA CCM MKOA WA MWANZA MIRAJI MTATURU AWAFUNZA VIONGOZI WA KISIASA NCHINI.

Miraji Mtaturu, Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza
Na:Shama Getrude
Viongozi wa vyama vya siasa nchini wametakiwa kuwatumikia wananchi bila kujali itikadi za aina yoyote hususani za kisiasa, ili kuendelelea kuidumisha amani iliyopo hapa nchini.

Kauli hiyo ilitolewa Jumamosi iliyopita na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu, katika mkutano wa hadhara wa chama hicho, uliofanyika Kata ya  Pansiasi Wilayani Ilemela.

Mtaturu alisema kuwa wapo baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa hapa nchini ambao wanawatumikia wananchi kwa ubaguzi wa itikadi za vyama vyao hivyo ni vyema wakaepukana na tabia hiyo ili amani iendelee kudumu nchini.

“Nawaombeni viongozi wa vyama vya siasa, watumikieni wananchi bila kujali itikadi za aina yoyote ikiwemo za kisiasa, kwani mkiwabagua amani haiwezi kuwepo nchini”. Alisema Mtaturu.

Hata hivyo alisema kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitaendelea kuwatumikia wananchi kwa kuwapatia huduma mbalimbali za Kimaendeleo bila kujali maeneo wanayoishi yanaongozwa na CCM au chama kingine cha Kisiasa.

“CCM itaendelea kuwaletea huduma mbalimbali bila kujali eneo mnaloishi linaongozwa na chama gani”. Alisema.

Naye Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Mwanza Simon Mangelepa alisema kuwa msingi mkubwa wa amani kuwa ni haki hivyo viongozi wa Kisiasa wanapowanyima haki wananchi wanaweza kusababisha vurugu  kutokea na hatimae kusababisha kupotea kwa amani nchini.

No comments:

Powered by Blogger.