LIVE STREAM ADS

Header Ads

TIGO NA HUAWEI WATOA MSAADA WA KOMPYUTA 25 HOSPITAL YA MKOA WA MWANZA SEKOUR TOURE.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Baraka Konisana (Kulia) akipokea Msaada wa Kompyuta 25 zenye Huduma ya Internet ya Bure bila Kikomo zilizotolewa na Kampuni za Tigo na Huawei katika Hospitali ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure jana. Kushoto ni Meneja Mkuu wa Kampuni ya Tigo nchini Diego Gutierrez.
Na:George GB Pazzo
Hospitali ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure inatarajia kuboresha huduma zake za utunzaji wa kumbukumbu za Wagonjwa  na Mapato, baada ya kupokea msaada wa Kompyuta 25 zilizotolewa na Kampyuni za Tigo na Huawei.

Hayo yalielezwa jana na Onesmo Rwakyendera ambae ni Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, wakazi wa zoezi la utoaji wa Kompyuta hizo lililofanyika hospitalini hapo.

Rwekyendera alibainisha kuwa awali hospitali hiyo ilikuwa ikitunza Kumbukumbu za Wagonjwa na Mapato katika Mfumo wa Makaratasi, jambo ambalo lilikuwa likisababisha ugumu na Usumbufu mkubwa katika utendaji wa kazi.

Aliutaja ugumu huo kuwa ni Kumbukumbu za wagonjwa kutopatikana kwa wakati pindi zinapohitajika kutokana na wingi wa Mafaili ya Wagonjwa hospitalini hapo, pamoja na upotevu wa Mapato kutokana na mkanganyiko wa taarifa zinazoandikwa kwenye karatasi.

“Tuna imani kuwa vifaa hivi vitatupatia taarifa kamili za mapato na matumizi ya kila siku, ambapo pia vitatupatia taarifa juu ya yale yanayoendelea katika ulimwengu wa matibabu ikiwa ni pamoja na utafiti na masomo kutoka maeneo mbalimbali”. Alisema Rwekyendera.

Ally Maswanya ambae ni Meneja wa Kampuni ya Tigo Kanda ya Ziwa alibainisha kuwa Komputa zilizotolewa hospitalini hapo zina thamani ya takribani Shilingi Milioni Thelathini ambapo zitakuwa na huduma ya Intaneti ya Bure bila Kikomo, huku akilitaja lengo la msaada huo ni kuhakikisha kuwa Utunzaji wa Kumbukumbu unaboreshwa zaidi hospitalini hapo.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Baraka Konisaga ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana alibainisha kuwa Serikali inatambua mchango wa Sekta binafsi hapa nchini katika kuboresha huduma za Kijamii huku akiongeza kuwa Msaada wa Kompyuta uliotolewa na Kampuni za Tigo na Huawei unaunga mkono juhudi za Serikali katika kutekeleza mpango wake wa Afya wa Mwaka 2013/18 ambao umelenga kuhakikisha kuwa huduma za Afya zinaingia katika mifumo ya Kidijitali.

Meneja Mkuu wa Kampuni ya Tigo nchini Diego Gutierrez alisema kuwa Msaada uliotolewa na katika Hospitali ya Sekour Toure ni katika Kutekeleza Mkakati wa Kampuni hiyo wa Kuyabadilisha maisha ya Watanzania katika sekta mbalimbali ambazo ni pamoja na Afya kuwa katika Mfumo wa Kidijitali.

Nae Afisa Mtendaji Mkuu wa Huawei Zhang Yongquan alisema kuwa msaada huo wa Komputa unaonyesha jinsi ambavyo Kampuni yake imejitolea katika Kusaidia Sekta ya Afya nchini ili kuendana na Mabadiliko ya Kiteknolojia.

Mwenyekiti wa Bodi wa Hospitali hiyo ya Sekour Toure Christopher Mwita Gachuma, alitoa rai kwa uongozi wa Hospitali hiyo kuhakikisha kwamba Komputa zilizotolewa na Kapuni za Tigo na Huawei zinatunzwa vizuri pamoja na zizitumia kwa ajili ya matumizi yaliyokusudiwa.
 Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga (Wa pili kulia) akimkabidhi Kaimu Mganga Mkuu Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Onesmo Rwakyendera (Mwenye Koti Jeupe) ikiwa ni msaada uliotolewa na Kampuni za Tigo na Huawei.
Kutoka kushoto ni Meneja Mkuu wa Kampuni ya Tigo nchini Diego Gutierrez, akifuatiwa na Mwenyekiti wa Bodi wa Hospitali ya Sekour Toure Christopher Mwita Gachuma, anaefuata ni Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga (Mtumishi wa Mungu), akifuatiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Huawei Zhang Yongquan na wa mwisho ni Kaimu Mganga Mkuu Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure Onesmo Rwakyendera.
Kutoka kushoto ni Meneja Mkuu wa Kampuni ya Tigo nchini Diego Gutierrez, akifuatiwa na Mwenyekiti wa Bodi wa Hospitali ya Sekour Toure Christopher Mwita Gachuma
Meneja wa Tigo Kanda ya Ziwa Ally Maswanya (Mwenye koti) akiwa na Wafanyakazi wengine wa Kampuni hiyo.
Wafanyakazi wa Tigo
Wafanyakazi wa Tigo na Huawei
Watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure
Watumishi wa Sekour Toure
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga (Mtumishi wa Mungu)
Neno kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga (Mwenye kinasa sauti).
Neno kutoka kwa Meneja Mkuu wa Kampuni ya Tigo nchini Diego Gutierrez (mwenye kinasa sauti).
Mwenyekiti wa Bodi wa Hospitali hiyo ya Sekour Toure Christopher Mwita Gachuma
Onesmo Rwekyendera ambae ni Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekour Toure.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Huawei Zhang Yongquan 
Meneja Mkuu wa Kampuni ya Tigo nchini Diego Gutierrez 
Ze Kompyutaz zilizotolewa na Kampuni za Tigo na Huawei
Picha ya Pamoja.
Special Thanks to Our Reader Nelson The Only One.

No comments:

Powered by Blogger.