LIVE STREAM ADS

Header Ads

BVR JIJINI MWANZA KUZUA MAANDAMANO.

Na:Elisa Anatory
Baadhi ya wakazi wa  Kata ya Buhongwa Jijini Mwanza wametishia kuandamana endapo kama wakazi wote wa Kata hiyo hawatapa fursa ya kujiandikisha katika zoezi la uandikishaji katika daftari la kudumu la wapiga kura kutokana na kasi ndogo ya zoezi hilo.

Jana wakazi hao walisema kuwa kasi ya uandikishaji inaenda taratibu kutokana na uchache wa Mashine za Biometric Voters Regstratin BVR pamoja na mashine hizo kupata hitirafu za mara kwa mara na hivyo kusababisha watu wengi kukaa katika foleni muda mrefu wakisubiri kuandikishwa.

Mwenyekiti  wa mtaa wa Buhongwa Magaribi Emanuel Mongo alisema kuwa juzi kulikuwa msururu wa watuzaidi ya 400 ila walioandikishwa ni watu 50 pekee ambapo jana kulikuwa na msururu wa watu zaidi ya 700 lakini hadi kufikia majira ya saa sita na nusu mchana watu takribani 60  ndio walikuwa wameandikishwa.

Kumekuwepo na Ushirikiano hafifu kati ya wasimamizi wakuu wa zoezi la Uandikishaji wa Wapiga Kura Jijini Mwanza, kwani licha ya kufuatwa mara kwa mara na wanahabari ili kujibu kero na malalamiko ya wananchi dhidi ya zoezi hilo, wamekuwa hawaonyeshi ushirikiano wowote zaidi ya kusema zoezi linakwenda vizuri.


Pamoja na Wilaya nyingine katika Mkoa wa Mwanza, zoezi la Uandikishaji Jijini Mwanza (Wilaya ya Nyamagana) lilianza June 09 katika Kata tano ambazo ni Rwanima, Mkuyuni, Buhongwa, Luchelele pamoja na Mkolani ambapo zoezi hilo linatarajia kukamilika june 15 mwaka huu na kuendelea katika Kata nyingine.

No comments:

Powered by Blogger.