DHANA POTOFU YASABABISHA WANANCHI KUTOTUMIA DARAJA LA MABATINI JIJINI MWANZA.
Na:George GB Pazzo
Licha ya Uwepo wa daraja la juu kwa ajili ya watembea kwa Miguu katika eneo la Mabatini Jijini Mwanza, bado wamekuwa wakisuasua kulitumia daraja hilo na hivyo kuhatarisha maisha yao kutokana na ajali za vyombo vya moto katika eneo hilo.
Licha ya Uwepo wa daraja la juu kwa ajili ya watembea kwa Miguu katika eneo la Mabatini Jijini Mwanza, bado wamekuwa wakisuasua kulitumia daraja hilo na hivyo kuhatarisha maisha yao kutokana na ajali za vyombo vya moto katika eneo hilo.
Wakizungumza
na Radio Metro kupitia Kampeni yake ya Kata kwa Kata, Mtaa kwa Mtaa, baadhi ya waendesha
pikipiki katika eneo hilo walisema kuwa wananchi wamekuwa hawatumii daraja hilo
kutokana na dhana potofu kwamba kuna mzunguko mrefu katika daraja hilo.
Walisema
kuwa kutokana na dhana hiyo potofu, kumekuwa na ajali za mara kwa mara katika
eneo hilo ambapo watembea kwa miguu wamekuwa wakigongwa na vyombo vya moto
pindi wanapokuwa wakijaribu kuvuka barabara bila kutumia daraja lililopo eneo
hilo.
Baadhi ya watumiaji
wa daraja hilo walisema kuwa hakuna mzunguko mrefu katika daraja hilo kama
inavyoelezwa na baadhi ya wananchi ambapo wamependekeza kuwa itungwe sheria
itakazowabana wale ambao hawazingatii matumizi ya daraja hilo.
Daraja la
Mabatini lilijengwa na Kampuni ya Nordic Construction Limited ya Tanzania kwa gharama
ya shilingi Milioni 899.025 kwa lengo la kupunguza kero ya msongamano wa magari
na ajali za mara kwa mara za watembea kwa miguu kugongwa na vyombo vya moto katika
eneo hilo la Mabatini, lakini baadhi ya wananchi wamekuwa hawaoni umuhimu wa
kulitumia jambo ambalo linahatarisha zaidi maisha yao kutokana na hatari ya
kugongwa na vyombo vya moto vinavyopita kwa kasi katika eneo hilo.
Credit:Radio Metro
Credit:Radio Metro
No comments: