LIVE STREAM ADS

Header Ads

CHAMA CHA ACT WAZALENDO CHAJINADI KUIONDOA CCM MADARAKANI.

Na: Elisa Anatory

Contact: 0763 34 50 64.
Katibu wa chama cha Alliance For Change and Transparency ACT Wazalendo Wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza Iddi Kiula amesema kuwa chama hicho kimejipanga kushika nyazifa mbalimbali za Uongozi katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu.

Kiula aliyasema hayo jana ofsini kwake wakati akizungumza na Binagi Media Group juu ya mikakati ya chama hicho katika kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu unaotarajiwa kufanyika Octoba 25.
     
Alisema kuwa chama hicho ambacho tangu kuanzishwa kwake kimekuwa kikivuna wanachama wa kutosha kila kukicha katika Wilaya ya Nyamagana, Mkoa wa Mwanza na Taifa kwa ujumla, kimenuwia kukiondoa madarakani Chama cha Mapinduzi CCM kuanzia ngazi ya Udiwani, Ubunge pamoja na Urais.

"Wale wenye sifa za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, fomu zinatarajiwa kuanza kutolewa kuanzia Julai Mosi hadi Julai 17 mwaka huu na gharama za uchukuaji fomu hizo ni Shilingi Elfu Kumi kwa ngazi ya Udiwani, Elfu Ishirini kwa Ubunge na Shilingi Laki Moja kwa nafasi ya Urais" Alisema Kiula.

Kiula alitanabaisha kwamba lengo la kuweka kiwango hicho ambacho kinaonekana ni kidogo ukilinganisha na vyama vingine kama CCM ambayo Fomu ya Urais ni shilingi Milioni Moja ni kutoa fursa kwa yeyote mwenye uwezo wa kuwa kiongozi kupata nafasi ya kugombea.

Akihitimisha mazungumzo na Binagi Media Group, Kiula aliwahimiza makada wa ACT Wazalendo wenye sifa za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu za kugombea ambapo aliwahakikishia kwamba anaamini chama hicho kitaibuka na ushindi mnono katika uchaguzi wa Mkuu wa Mwaka huu kutokana na sera zake imara ambazo zinakubaliwa na Watanzania walio wengi.

No comments:

Powered by Blogger.