LIVE STREAM ADS

Header Ads

DIWANI KATA YA MBUGANI JIJINI MWANZA AWAJIA JUU WANAOTANGAZA NIA YA KUGOMBEA KATIKA KATA HIYO.

Diwani wa Kata ya Mbugani Jijini Mwanza Hassan Kijuu (Kulia) akibonga na GB Pazzo (Kushoto).
Na:George GB Pazzo
Diwani wa Kata ya Mbugani Jijini Mwanza (Chadema) Hassan Hashim Kijuu ameelezea kuwashangaa baadhi ya wanachama wa chama chake wanaojitokeza na kutangaza nia ya kugombea katika Kata hiyo wakati bado yuko madarakani.

Kijuu alitoa Kauli hiyo juzi alipokuwa akizungumza na Mtandao huu ambapo alibainisha kwamba, kwa mjibu wa kanuni za chama chake (Chadema), mtangaza nia hapaswi kutangaza kugombea ili hali ukomo wa kiongozi alie madarakani bado haujafikia mwisho.

Kijuu alisema kuwa anashangazwa na Chama chake kukaa kimya wakati kanuni zinaendelea kuvunjwa kutokana na maadhi ya makada katika Kata ya Mbugani kutangaza nia ya kugombea udiwani huku yeye akiwa bado madarakani.

Alisema kuwa kanuni za chama zinaeleza wazi kuwa yeyote atakaetangaza nia ya kugombea wakati nafasi ya uongozi anayoitaka bado inashikiliwa na kiongozi alie madarakani, mtu huyo ni sharti fomu yake izuiliwe ili asiweze kugombea.

Aidha alisema kuwa hana shaka na nafasi yake ya udiwani kwa kuwa diwani wa Kata ya Mbugani katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu anamjua Mungu hivyo hana wasiwasi na wote waliotangaza nia ya kugombea katika Kata hiyo.

Tayari Makada kadhaa ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA katika Kata ya Mbugani wametangaza nia ya Kugombea udiwani katika Kata hiyo, ambapo miongoni mwa makada hao ni pamoja na Mwenyekiti wa Mtaa wa Unguja Richard Daniel Kajuna.
BONYEZA PLAY HAPA CHINI KUSIKILIZA

No comments:

Powered by Blogger.