LIVE STREAM ADS

Header Ads

HII NDIYO KAULI YA CCM MKOANI MWANZA KUHUSIANA NA ZOEZI LA UANDIKISHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA.

Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu (Mwenye Miwani akiwasili katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza juzi jumamosi.
 Na:George GB Pazzo
Wananchi Mkoani Mwanza wameshauriwa kujitokeza kwa Wingi kwa ajili ya Kujiandisha katika daftari la Kudumu la Wapiga Kura ili kupata sifa ya kushiriki katika zoezi la Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi August Mwaka huu.

Ushauri huo umetolewa na Katibu wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mwanza Miraji Mtaturu, wakati akiwahutubia wananchi katika Mkutano wa hadhara uliofanyika juzi katika Uwanja wa Mbugani Jijini Mwanza.

Mtaturu ametoa rai kwa kila mwananchi aliefikisha Umri wa Miaka 18 na kuendelea kuhakikisha kuwa anajiandikisha katika daftari la kudumu la Wapiga Kura, lengo likiwa ni kutumia haki yake ya Kikatiba ya kuwachagua viongozi atakaoshirikiana nao katika shughuli za kimaendeleo.

Kwa upande wake Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana Elias Mpanda amewasihi wanasiasa kuacha kuwagombanisha wananchi kutokana na itikadi za Kivyama katika kipindi hiki cha kuelekea katika Uchaguzi Mkuu ambapo amewasihi wanasiasa wenye tabia hiyo kuwa na siasa za kiustarabu wawapo Majukwaani.

Nae John Lipes Kayombo ambae ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC) anaewakilisha Vyuo Vikuu nchini, amewasihi wanafunzi wote wa Vyuo Vikuu nchini kuwa watulivu na kuachana na Migomo isiyo na tija katika kipindi hiki cha kuelekea katika Uchaguzi Mkuu ambapo amebainisha kuwa tayari kuna mipango madhubuti ya kuhakikisha kuwa wanafunzi ambao hawajapata mikopo yao wanapata mikopo hiyo kwa wakati.

Kwa mjibu wa ratiba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini, zoezi la uandikishaji wa wananchi katika daftari la kudumu la wapiga kura linatarajiwa kuanza kesho June Mbili katika Mikoa ya Geita, Mwanza, Shinyanga na Simiyu ambapo litafikia tamati Julai Nne mwaka huu.
John Lipes Kayombo ambae ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC) anaewakilisha Vyuo Vikuu nchini
Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana Elias Mpanda (Kushoto) akifuatiwa na Hussein Kim ambae ni Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Nyamagana (Katikati) pamoja Henry James ambae pia ni Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Ilemela.
Wananzengo!

No comments:

Powered by Blogger.