MAKAMBA AWAUMBUA WANAOTUMIA KIGEZO CHA GESI KUOMBA RIDHAA YA URAIS.
Mbunge wa Jimbo la Bumbuli Mkoani Tanga ambaye pia ni Naibu Waziri wa Sayansi na Teknologia January Makamba akitangaza jana nia ya kugombea Urais (CCM) katika Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam.
Na: ELISA
ANATORY 0763345064
EMAIL: anatoryelisa@gmail.com.
Mbunge wa Jimbo la
Bumbuli Mkoani Tanga ambaye pia ni Naibu Waziri wa Sayansi na Teknologia
January Makamba ametangaza rasmi nia ya kugombea nafasi ya urais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi CCM.
Akitangaza
nia hiyo jana Jijini Dar es salaam, Makamba alisema kuwa ili Tanzania iweze
kupiga hatua kimaendeleo, ni lazima iwe na kiongozi shupavu, mwaminifu, mwenye
busara, mwenye ujuzi na uzoefu katika kuliongoza Taifa.
Makamba
alitaja baadhi ya vitu ambavyo atavipa kipau mbele pale atakapopewa na fasi
hiyo kuwa ni pamoja na kutokomeza ufisadi, rushwa, kupambana na umaskini pamoja
na maadili kwa viongozi hapa nchini.
Aidha
aliongeza kuwa atahakikisha anafufua viwanda vilivyokufa kutokana na ukosa mali
ghafi, kutoa mikopo ya kutosha kwa wanafunzi wa Vyuo Vikuu ili uongeza kiwango
cha elimu, ikiwa ni pamoja na kuinua kiwango cha elimu kote nchini
ikilinganishwa na ilivyo sasa.
Kuhusu
mapato ya gesi Makamba aliwataka watanzania kuachana na baadhi ya wagombea wanaosema
kuwa watakapoingia madarakani katika kipindi cha miaka mitano nchi itanufaika
na nishati ya gesi ambapo alibainisha kuwa nishati hiyo itaanza kulinufaisha
taifa baada ya miaka kumi ijayo.
Makada wa CCM na Wananchi wakimsikiliza January Makamba katika Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es salaam jana.
No comments: