MMOJA AFARIKI DUNIA HUKU WENGINE WAKINUSURIKA BAADA YA KUBUGIA CHAKULA CHENYE SUMU.
Na:Ofisi ya RPC Mara
Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la
Ghati Itumbo amefariki dunia katika
kijiji cha Maji Moto wilaya ya Serengeti
Mkoani Mara, baada ya kula
chakula kinacho sadikiwa kuwa na sumu katika mgahawa mmoja uliokuwa
ukiuza chakula Kijijini hapo.
Kaimu
kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Mara Ernest Kimora aliyasema hayo juzi wakati
akitoa taarifa kwa vyombo vya habari ambapo aliongeza kuwa katika tukio
hilo pia kuna watu watatu walinusurika kifo baada ya kula chakula
hicho.
Aliwataja
walionusurika kuwa ni Elizabeth Juma, Pendo Mussa pamoja na Neema Nelson ambapo
wote wamelazwa katika hospitali ya DDH Mugumu ya Mkoani humo kwa ajili ya
matibabu.
Alisema
hakuna yeyote aliekamatwa kuhusiana na tukio hilo na kuongeza kuwa jeshi la
polisi Mkoani Mara linaendelea na uchunguzi wake ili kubaini waliohusika ambapo
alibainisha kwamba mabaki ya chakula kilicholiwa na watu hao yamechukuliwa
kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Hata hivyo
Kaimu Kamanda Kimora aliwaasa wananchi kuepukana na tabia ya kula vyakula ovyo katika maeneo yasiyo rasmi
hususani katika maeneo yenye mikusanyiko
wa watu ili kuepukana na athari zinazoweza kuwakumba.
No comments: