UONGOZI WA KATA YA MBUGANI JIJINI MWANZA WAKIRI MAPUNGUFU KATIKA ZAHANATI YAKE.
Diwani wa Kata ya Mbugani Hassan Kijuu (Kulia) akibonga na Alphonce Tonny Kapela (Kushoto) @Metro FM.
Na:George GB Pazzo
Uongozi wa Kata ya Mbugani Jijini
Mwanza umekiri kuwepo kwa changamoto mbalimbali katika Zahanati ya Kata hiyo
huku ukibainisha kuwa changamoto hizo haziwezi kutatuliwa kwa sasa kutokana na
ukubwa wake.
Diwani wa
Kata ya hiyo Hassan Hashim Kijuu (Chadema) alitoa kauli hiyo wiki iliyopita wakati akijibu
malalamiko ya wananchi wa Kata hiyo ambao waliyatoa wakati wakizungumza katika
Kampeni ya Mtaa kwa Mtaa inayoendeshwa na Radio Metro Fm.
Kijuu alisema
kuwa licha ya wananchi kulalamikia za afya zinazotolewa katika Zahanati hiyo,
pia inakabiriwa na ukosefu wa barabara inayoweza kupitisha gari au pikipiki kwa
ajili ya kusaidia wagonjwa kufika katika Zahanati hiyo kupaya matibabu.
Alikiri kuwa
hakufurahishwa na Zahanati hiyo kujengwa katika eneo lenye mwinuko na hivyo
kusababisha changamoto za miundombinu ambapo alibainisha kuwa zinahitajika
zaidi ya shilingi Milioni Mia nane kwa ajili ya kukarabati barabara inayoelekea
katika zahanati hiyo.
“Kwa kuwa nimeombwa
na wananchi wa Kata ya Mbugani kutetea nafasi yangu ya Uongozi, changamoto hiyo
pamoja na nyingine ambazo ambazo hazijatatuliwa zitatafutiwa ufumbuzi katika
awamu ijayo ya uongozi baada ya uchaguzi”Alisema Kijuu.
Katika hatua
nyingine Kijuu alizungumzia changamoto ya Mafuriko katika eneo la Mabatini
ambapo alibainisha kuwa bado kuna changamoto ya kuwahamisha wananchi waliojenga
katika eneo hilo kwa kuwa wananchi wanapaswa kupewa maeneo mbadala kwa ajili ya
makazi yao kabla ya kuhamishwa.
Aidha alikiri
maisha ya wakazi wa Mtaa wa Nyerere B kuwa hatarini kutokana na hatari ya
nyumba zao kuporomokewa na Jiwe lililopo katika Mtaa huo, ambapo alisema kuwa
suala hilo bado linakwamishwa na Viongozi wa Serikali ambao wamekuwa wazito
katika kuhakikisha kuwa jiwe hilo linapasuliwa kabla halijasababisha madhara
kwa wananchi.
“Mkuu wa
Mkoa alithubutu kuniuliza kuwa kati ya Mawe na Watu kipi kilitangulia, akasema
kama mawe ndiyo yalitangulia basi watu ndio wahame. Sasa watu wanahama kwenda
wapi na wakati wanajenga Serikali ilikuwa inawaangalia tu. Tathmini
iliyofanyika iligharimu kama Milioni Kumi na tano sasa hiyo nguvu ndiyo bado
inasuasua”.Alisema Kijuu.
Hivi majuzi Wananchi wa Kata ya Mbugani na Mabatini walilalamikia Ukosefu wa
huduma bora katika Zahanati yao ya Mbugani kutokana na uhaba wa dawa pamoja na
miundombinu isiyofikika Zahanatini hapo huku wale wanaoishi katika Mtaa wa
Nyerere B wakielezea hofu yao kutokana na Jiwe lililopo katika Mtaa huo ambao
uko Kilimani ambalo liko hatarini kuporomokea nyumba zaidi ya 13 katika Mtaa
huo.
No comments: