ZOEZI LA UANDIKISHAJI JIJINI MWANZA LAKABILIWA NA CHANGAMOTO KUBWA.
Na:Elisa Anatory
Wakazi
Jijini Mwanza wameilalamikia serikali kwa
kutoa mashine chache za uandikishaji za Biometrick Voters Registration BVR pamoja na kutowatangazia wakazi hao juu ya tarehe rasmi ya zoezi la uandikishaji
katika Mitaa yao.
Wakizungumza na Redio Metro Fm kwa nyakati tofauti wakazi wa Kata za Buhongwa, Rwanima, Luchelele, Mkolani pamoja
na Mkuyuni walisema kuwa mashine hizo
zimeonyesha mapungufu makubwa na hivyo kushindwa kufanya kazi kwa ufasaha.
“Jamani wengine sisi ni wajawazito hivyo tunavyoendelea kusukumana
na hili jua mbona mimba zetu zitatoka?”. Zilisikika sauti za akina mama
waliokuwa katika foleni ya kujiandikisha katika Kituo cha Shule ya Sekondari Mkolani
kilichopo Kata ya Mkolani Jijini Mwanza.
Katika Kituo hicho kulizuka taflani wakati wa zoezi la uandikisha hii leo baada ya utaratibu wa kufuata mstari kuvurugika kutokana na kila mmoja kutaka kumtangulia mwenzake katika kujiandikisha hii ikiwa ni baada ya mashine iliyokuwa ikitumika katika kituo hicho kuharibika na zoezi kusimama kwa muda.
Katika Kituo hicho kulizuka taflani wakati wa zoezi la uandikisha hii leo baada ya utaratibu wa kufuata mstari kuvurugika kutokana na kila mmoja kutaka kumtangulia mwenzake katika kujiandikisha hii ikiwa ni baada ya mashine iliyokuwa ikitumika katika kituo hicho kuharibika na zoezi kusimama kwa muda.
Aidha wakazi hao waliiomba Tume ya Taifa ya uchaguzi NEC kuongeza
vifaa vya kutosha ikiwa ni pamoja na kuweka mashine tatu kwa kila kituo ili kuraisisha
zoezi hilo ambapo waliongeza kuwa hilo lisipofanyiwa kazi litasababisha watu
wengi kutojisajili katika daftari la kudumu la wapiga kura.
Charles Nkonga Mwenyekiti Mtaa wa Ibanda katika Kata Mkolani Jijini
Mwanza alikiri kuwepo kwa tatizo la BVR kuharibika huku akibainisha kuwa zoezi
la uandikishaji katika Mtaa wake limechelewa kuanza kutokana na mashine hizo kuchelewa
kufikishwa katika vituo vya Kujiandikishia.
Kama ilivyo katika Wilaya za Mkoa wa Mwanza, zoezi la Uandikishaji
katika Wilaya ya Nyamagana (Jijini Mwanza) limeanza rasmi hii leo June 09, 2015
katika Kata tano ambazo ni Buhongwa, Rwanima, Luchelele, Mkolani pamoja na Mkuyuni
na linatarajiwa kufikia tamati June 15, 2015 ambapo litadumu kwa muda wa siku
saba na baada ya hapo litaendelea katika
Kata nyingine.
Credit:Radio Metro
Credit:Radio Metro
No comments: