LIVE STREAM ADS

Header Ads

LEMBELI NA BULAYA WAPOKELEWA VYEMA JIJINI MWANZA. CHADEMA WASEMA MGOMBEA URAIS ATATOKA UKAWA.

Mamia ya Wananchi wakiwa katika Mkutano wa Chadema uliofanyika jana Jijini Mwanza.
Na:George GB Pazzo
Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kimesema kuwa mazungumzo miongoni mwa Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi UKAWA bado yanaendelea, lengo likiwa ni kufikia maridhiano ya pamoja na hatimae kumsimamisha Mgombea mmoja wa nafasi ya Urais kupitia Umoja huo katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe alitoa kauli hiyo jana Katika Uwanja wa Magomeni Kirumba Jijini Mwanza, wakati akihutubia mamia ya wananchi katika Mkutano wa hadhara wa kuwapokea aliekuwa Mbunge wa Kahama James Lembeli pamoja na Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Mara Ester Bulaya wote kutoka Chama cha Mapinduzi CCM ambao wamejiunga na Chadema.

Mbowe alisema kuwa viongozi wa vyama vinavyounda Umoja huo wanafanya juhudi zote ili kuhakikisha kwamba maridhiano yanapatikana miongoni mwao na hatimae kufanikisha kumsimamisha mgombea mmoja wa Urais kwa niaba ya vyama vyote hivyo wananchi wawe na subira wakati mazungumzo yanaendelea.

“Naomba wananchi muwe na Utulivu maana Umoja wetu wa Ukawa ni wa Msingi sana hivyo tusiwe na haraka wala tusiwe na mihemuko. Tutambue kwamba kuna changamoto zinapatikana lakini sisi kama viongozi tunawahakikishia kwamba tutatumia kila mbinu na kila goti litapigwa kuhakikisha kuwa Ukawa tunamaliza salama majadiliano yetu na tunakuwa na mgombea mmoja kwa niaba ya vyama vyote baada ya kuridhiana”. Alismema Mbowe huku akishangiliwa na umati wa Wananchi waliokuwa katika Mkutano huo.

Hata hivyo mkutano huo ulifanyika huku Viongozi wa Vyama vingine vinavyounda Umoja huo wa Ukawa ambavyo ni Chama cha Wananchi CUF, NCCR Mageuzi pamoja na NLD wakishindwa kuhudhuria licha ya kupewa mwaliko, ambapo Mbowe alisema kuwa hali hiyo ilisababishwa na mwingiliano shughuli za kichama ndani ya vyama hivyo.

“Leo asubuhi ilikuwa nije na Mzee Makaidi (Emmanuel Makaidi Mwenyekiti wa NLD) lakini kwa bahati mbaya kutokana na foleni za Dar es salaam akachelewa ndege, niliongea na Mh.Lipumba (Profesa Ibrahim Lipumba Mwenyekiti wa CUF) na Mbatia (James Mbatia Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi) lakini nao walikuwa na vikao vya ndani ya vyama vyao kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi hivyo wakashindwa kufika”. Alitanabaisha Mbowe huku akiwahimiza watanzania kuwa wavumilivu juu ya kiu yao kutaka kumjua Mgombea Urais atakae uwakilisha Ukawa kwa kusema kuwa mgombea huyo atatangazwa muda mwafaka utakapofika.


Kwa pamoja Ester Bulaya ambae alikuwa Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) akiwakilisha Vijana Mkoani Mara na James Lembeli ambae alikuwa Mbunge wa Kahama (CCM) baada ya kupokea kadi ya Chadema walisema kuwa wakati umefika wa Watanzania kufanya mabadiliko kwa kuhakikisha kuwa wanaiondoa CCM Madarakani kwa kuwa imeshindwa kutumia rasrimali zilizopo nchini kuwaletea maendeleo.

“Nikamtoeee nisimtoeeeee…Kamtoeeee…Naniiiii…Wasiraaaaa…Wapiii…Bundaaaaaa…linii tarehe Octoba 25…Kama anasikia atafuata ushauri wa Makongoro Nyerere kwamba awamu ya Kwanza yupo, ya pili yupo, ya tatu yupo, ya nne yupo, lakini awamu ya tano bye bye”. Alisema Bulaya ikiwa ni tahadhari kwa Mbunge Jimbo la Bunda Mkoani Mara (CCM) Mh.Steven Wasira ambae pia ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika.
Hali ilivyokuwa Katikati ya Jiji la Mwanza jana baada ya Mkutano wa Chadema Kumalizika ambapo wanachadema walisindika msafara wa viongozi wa Chama hicho hadi hotelini.
Powered by Blogger.