RUNINGA UPANDE WA DEREVA KATIKA DALADALA HII, NI HATARI KWA USALAMA WA ABIRIA NA WATUMIAJI WENGINE WA BARABARA.
Habari za Wakati huu wapendwa wasomaji Wa Binagi Media Group. Ni matumaini yetu ya Kwamba mtandao huu unasomwa na watu mbalimbali wakiwemo Madereva, Abiria na hata maaskari wa Usalama barabarani.
Kwa mantiki hiyo leo tunaweka pembeni mbwembe zetu za uandishi na kuungana live na mmoja wa wasomaji wetu ambae anatueleza moja ya tabia ambazo si nzuri zinayofanywa na baadhi ya madereva Jijini Mwanza na hivyo kuhatarisha usalama wa abiria na baada ya hapo tutafute suluhisho juu ya tatizo hilo iwe ni kwa vitendo au ushauri.
Kwa mantiki hiyo leo tunaweka pembeni mbwembe zetu za uandishi na kuungana live na mmoja wa wasomaji wetu ambae anatueleza moja ya tabia ambazo si nzuri zinayofanywa na baadhi ya madereva Jijini Mwanza na hivyo kuhatarisha usalama wa abiria na baada ya hapo tutafute suluhisho juu ya tatizo hilo iwe ni kwa vitendo au ushauri.
Inaanzia hapa "Kuna daladala moja
nimepanda leo ya kutoka Kishiri kuelekea Airport (Kisesa-Mecco-Airpot yenye nambari T 778 CLL). Ndani ya gari hiyo kuna Tv
mbili, moja ni kubwa ambayo abiria wote tunaweza tizama na nyingine ni kadogo
sana kapo pale mbele kwa dereva.
Kitu ambacho
kimenifanya niwashirikishe wenzangu ni kwamba huyo dereva alikuwa anatizama
kale katv kadogo huku anaendesha gari, ilifikia wakati kidogo aigonge gari ya
mbele maana alikuwa busy anatizama tv.
Haikuishia hapo
tulipofika maeneo ya ghana tena akafunga break ghafla kwa sababu ile ile.
Jamani kwa mazoea
haya hv ajali zitapungua kweli? Abiria tumemwambia sana lakini hajatilia
maanani.
Nimebahatika kupiga
picha namba za gari ili tusaidiane kukOmesha matatizo haya". Anamaliza kusimulia.
Karibuni kwa ushauri na msaada zaidi...
No comments: