LIVE STREAM ADS

Header Ads

VIONGOZI WA CHAMUITA KANDA YA ZIWA WATAMBULISHWA RASMI.

Viongozi wa CHAMUITA ambapo kutoka Kushoto ni Mjumbe Sospeter Tawo, Katibu Mwenezi Taifa Stella Joel, Katibu Mwenezi Kanda ya Ziwa Maganga James Gwensaga, Mkurugenzi wa Itifaki Taifa Magreth Sembuche, Katibu Mwanza Vanessa Laban, Mjumbe Taifa Ulimbaga Mwakatobe na Makamu Mwenyekiti Kanda ya Ziwa Emmanuel Mwakisepe wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kuwatambulisha viongozi wa chama hicho Kanda ya Ziwa jana.
 Na:George GB Pazzo
Chama cha Muziki wa Injili Tanzania CHAMUITA jana kimewatamulisha rasmi Viongozi wake wa Kanda ya Ziwa, ambao watashirikiana na Waimbaji wa Muziki huo ili kuhakikisha kuwa Waimbaji hao wananufaika na kazi  zao.

Kabla ya Viongozi hao kutambulishwa katika kikao kilichofanyika Jijini Mwanza, Katibu Mwenezi wa Chama hicho Taifa Stella Joel alisema kuwa lengo Kuu la Chama hicho ambacho kilianzishwa mwaka 2011 ni kuwaweka wanamuziki wa Muziki wa Injili pamoja kwa ajili ya kutetea haki zao na hatimae kunufaika na muziki wao.

“Lengo la Chama hiki cha Muziki wa Injili Tanzania ni kuwaweka wanamuziki pamoja ili tuweze kuwa na sauti moja ya kutuwezesha kutetea na kunufaika na kazi zetu, kama tunavyoona sasa hivi Muziki wa Injili unazidi kukua na kuna pesa nyingi ambayo inapatikana lakini haiwafikii wanamuziki wa injili". Alisema Joel na kuongeza; 

"Kwa Mfano sasa hivi kuna kazi nyingi zinauzwa kwa njia ya mtandao kama vile kuna Youtube, Miito ya Simu, Muziiki, Mkito na nyinginezo ambapo njia hizo zinaingiza mabilioni ya pesa, na ndiyo maana tuliona kuna umuhimu wa kuanzisha chama hiki kwa ajili ya kusimamia na kulinda haki zetu”. Alibainisha Joel ambae pia ni mwimbaji wa Muziki huo wa injili.

Viongozi waliotambulishwa na chama hicho kwa ajili ya Kusimamia shughuli zake Kanda ya Ziwa ni Mwenyekiti Emmy Lema, Makamu Mwenyekiti Emmanuel Mwakisepe, Katibu Vanessa Laban, Katibu Mwenezi Maganga Gwensaga pamoja na Mweka Hazina Sarah Gagala.

Akizungumza mara baada ya Utambulisho huo, Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Kanda ya Ziwa Emanuel Mwakisepe, aliwahimiza wanamuziki wa Muziki wa Injili kujiunga nacho kwa ajili ya kunufaika na manufaa yake ambayo ni pamoja na kuwasaidizi kusajili wa nyimbo zao pamoja na chama kusimamia taratibu za kufuata ili kunufaika na nyimbo zao pindi zinapokuwa zikitumika katika mitandao mbalimbali ikiwemo miito ya simu na hata kuunganishwa na wasambazaji wa muziki huo.

Nae Katibu Mwenezi wa CHAMUITA Kanda ya Ziwa Maganga Gwensaga alisema kuwa chama hicho ndicho chama pekee ambacho kinatambulika nchini kwa ajili ya kutetea haki na maslahi ya waimbaji wa muziki huo ambapo alitanabaisha kwamba pia kinatambulika na Shirikisho la Vyama vya Muziki nchini hivyo waimbaji wa Muziki huo wakitumie kwa ajili ya kufahamu masuala yao mbalimbali ambayo yatawasaidia kunufaika na kazi zao.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Itifaki wa CHAMUITA Taifa Magreth Sembuche aliwaomba wadau mbalimbali ambao ni pamoja na wachungaji na wadhamini kujiunga na chama hicho kupitia uanachama wa heshima lengo likiwa ni kukisaidia kufikia malengo yake ambayo ni pamoja na kuanzisha redio kwa ajili ya kucheza muziki wa njili, lakini pia kufungua maduka katika maeneo mbalimbali nchini yatakayokuwa yakiuza muziki huo jambo ambalo litasaidia wanamuziki wa injili kunufaika na kazi zao zaidi.


Kwa wanamuziki wa Injili pamoja na Wadau mbalimbali waliopo Kanda ya Ziwa ambao wanapenda kujiunga na CHAMUITA, wanahimizwa kuwasiliana na Katibu Mwenezi ambae ni Maganga Gwensaga kwa nambari +255 (0) 756 20 78 92 kwa ajili ya maelekezo na utaratibu zaidi.
Viongozi wa CHAMUITA ambapo kutoka Kushoto ni Mjumbe Sospeter Tawo, Katibu Mwenezi Taifa Stella Joel, Katibu Mwenezi Kanda ya Ziwa Maganga James Gwensaga, Mkurugenzi wa Itifaki Taifa Magreth Sembuche, Katibu Mwanza Vanessa Laban, Mjumbe Taifa Ulimbaga Mwakatobe na Makamu Mwenyekiti Kanda ya Ziwa Emmanuel Mwakisepe wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kuwatambulisha viongozi wa chama hicho Kanda ya Ziwa jana.
Kikao Kikiendelea
Majadiliano yakiendelea
Ni hoja juu ya Hoja kwa watumishi hawa wa Mungu kupitia Uimbaji
Kikao cha CHAMUITA Kanda ya Ziwa.
Kikao cha CHAMUITA Kanda ya Ziwa.
Kikao cha CHAMUITA Kanda ya Ziwa.
Kikao cha CHAMUITA Kanda ya Ziwa.
Kikao cha Chama cha Kuwatambulisha viongozi wa Muziki wa Injili Tanzania wanaowakilisha Kanda ya Ziwa kilifanyika jana Vinazo Hotel Jijini Mwanza.

No comments:

Powered by Blogger.