WATU WENYE ULEMAVU WILAYANI NYAMAGANA WASHINDWA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI KUTOKANA NA GHARAMA ZA UCHAGUZI.
Katibu wa Chama hicho Omari Matajago Sendama (Kulia) akizungumza na GB Pazzo @Metro Fm & Binagi Media Group (Kushoto).
Na:George GB Pazzo
Chama cha Watu wenye Ulemavu CHAWATA Wilaya
ya Nyamagana Mkoani Mwanza, Kimesema kuwa Watu wenye ulemavu wameshindwa
kujitokeza kwa ajili ya kuwania kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika
Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, kutokana na kushindwa kumudu gharama za uchaguzi
ndani ya yama vya Siasa.
Katibu wa
Chama hicho Omari Matajago Sendama aliyasema hayo jana wakati akizungumza na
Radio Metro, juu ya ushiriki wa watu wenye ulemavu katika kuwania nafasi za
uongozi na namna watu hao walivyoshiriki katika zoezi la uandikishaji wa wapiga
kura lililomalizika hivi karibuni Mkoani Mwanza.
Sendama
alisema kuwa katika zoezi la Uandikishaji Wilayani Nyamagana, hakukuwa na
malalamiko yoyote kutoka kwa watu wenye ulemavu kwa kuwa watu hao walikuwa
wakipewa kipaumbele zaidi hali iliyopelekea mwamko wao katika kujiandikisha kuwa
mkubwa.
Kuhusiana na
ushiriki wa watu wenye ulemavu katika kuwania nafasi za uongozi Wilayani
Nyamagana, Sendama alibainisha kuwa ofisi yake haijapokea jina lolote la mtu
mwenye ulemavu ambae amejitokeza kwa ajili ya kuwania nafasi ya kugombea
uongozi wowote ule kutokana na kushindwa kumudu gharama za uchaguzi zinazotozwa
na vyama vya siasa hapa nchini.
Alisema kuwa
awali baadhi ya walemavu walikuwa wakijitokeza kwa ajili ya kuwania kugombea
nafasi mbalimbali za uongozi, lakini jitihada zao zilikuwa zikishindikana
kutokana na kushindwa kulipia gharama za kampeni ambazo mgombea hutakiwa
kuzilipa ambapo ameongeza kuwa watu wenye ulemavu wanaomba utaratibu huo
kubadilika na badala yake wapewe fursa ya kugombea bila kuwepo kwa gharama
zozote.
Kwa pamoja
Christina Mnana Mwiye ambae ni Mjumbe wa CHAWATA Mkoa wa Mwanza pamoja na
Rehema Idd ambae ni Mratibu wa Kikundi cha akinamama wenye Ulemavu Wilaya ya
Nyamagana cha Disability Dream Pilot Project walisema kuwa mbali na watu wenye
ulemavu kushindwa kumudu gharama za uchaguzi, pia wanakabiriwa na changamoto
nyingi ambazo ni pamoja na kukosa kuaminiwa na wapiga kura kwa minajiri kuwa hawawezi
kuwa viongozi.
Walisema
kuwa bado wanakabiliwa na ukosefu wa mazingira bora ya kupata elimu hali ambayo
inawafanya kukosa fursa za kuwania nyazfa za uongozi ambapo wamehimiza kuwa
viongozi watakaochaguliwa katika uchaguzi wa mwaka huu wanapaswa kuhakikisha
kuwa wanawasemea wanapata haki zao za msingi ambazo ni pamoja na kupata elimu
na kushirikishwa katika uteuzi wa nafasi mbalimbali za uongozi.
Hata hivyo licha ya CHAWATA Wilaya ya Nyamagana kubainisha kuwa hakuna mlemavu yeyote aliejitokeza kugombea katika uchaguzi wa Mwaka huu, Radio Metro Fm imebaini kwamba yupo mmoja ambae amejitosa kuwania kuteuliwa na Chama cha Mapinduzi CCM ili kugombea ubunge Jimbo la Nyamagana.
Hata hivyo licha ya CHAWATA Wilaya ya Nyamagana kubainisha kuwa hakuna mlemavu yeyote aliejitokeza kugombea katika uchaguzi wa Mwaka huu, Radio Metro Fm imebaini kwamba yupo mmoja ambae amejitosa kuwania kuteuliwa na Chama cha Mapinduzi CCM ili kugombea ubunge Jimbo la Nyamagana.
Katibu wa Chama hicho Omari Matajago Sendama (Kulia) akizungumza na GB Pazzo @Metro Fm & Binagi Media Group (Kushoto).
Christina Mnana Mwiye ambae ni Mjumbe wa CHAWATA Mkoa wa Mwanza
Rehema Idd ambae ni Mratibu wa Kikundi cha akinamama wenye Ulemavu Wilaya ya Nyamagana cha Disability Dream Pilot Project.
No comments: