LIVE STREAM ADS

Header Ads

WAZEE WA KATA YA MBUGANI JIJINI MWANZA WAHIMIZA USHINDI NA MSHIKAMANO NDANI CCM.

Kikao cha Wazee na Vijana wa CCM Kata ya Mbugani Jijini Mwanza kilichokutana jana Aspen Hotel ili kutafuta Mshikamano ndani ya Chama chini ya Uongozi wa Wazee wa Kata hiyo.
 Na:George GB Pazzo
Uongozi wa Wazee wa Kata ya Mbugani Jijini Mwanza umewahimiza Wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Kata hiyo kuondoa tofauti zao za Kisiasa na badala yake waungane kwa pamoja ili kuhakikisha kuwa chama hicho kinaibuka na ushindi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

Uongozi huo ulitoa kauli hiyo jana kupitia kwa Mwenyekiti wake Mzee Joseph Daniel katika kikao kilichofanyika Aspen Hotel Jijini Mwanza, kikiwa kimewakutanisha Wazee pamoja na Vijana wa CCM kutoka Kata hiyo ya Mbugani.
 Mzee Daniel alisema kuwa mshikamano ndani ya CCM katika Kata hiyo umepotea, hali ambayo ilipelekea chama kupotea ushindi katika Uchaguzi wa Mwaka 2010 na hivyo kuwachanganya wanaccm hususani Wazee wa Chama.

Alisema baada ya hali hiyo kujitokeza, Wazee na Vijana wa CCM Kata ya Mbugani waliamua kutafuta mshikamano ndani ya Chama kupitia kwa Uongozi huo wa Wazee wa Kata ya Mbugani.

“Mshikamano ndani ya chama hivi sasa haupo na hali hii imepelekea Kata yetu kupoteza udiwani na hivyo kuongozwa na upinzani. Ni kutokana na hilo, wazee wa CCM na Vijana wa CCM wameamua kutafuta mshikamano ndani ya chama ili kuhakikisha umoja unaimalika na kukiwezesha chama kuibuka na ushindi katika uchaguzi wa mwaka huu kwa ngazi ya Udiwani, ubunge pamoja na Urais”. Alisema Mzee Daniel ikiwa ni nukuu aliyoisoma kutoka katika barua iliyoandikwa na Wazee na Vijana wa CCM Kata ya Mbugani.


Kwa pamoja kikao hicho kupitia kwa wachangiaji mbalimbali akiwemo Mzee Benedict Pamba, Aman Mussa, Ally Kashumali, Halima Mbomba na Vijana Ally Msoya, Adroph Charles, Shaban Majuto, Mohamed Khamis pamoja na Faustine Atanas kiliazimia kwamba Umoja na Mshikamano ndani ya CCM vinapaswa kuimalishwa ili kuhakikisha kwamba chama kinarudisha heshima yake kwa kuibuka na ushindi katika Uchaguzi wa Mwaka huu.
Kutoka Kushoto ni Faustine Atanas ambae ni Mwenyekiti wa UVCCM Kata ya Mbugani, Katikati ni Joseph Daniel ambae ni Mwenyekiti wa Wazee Kata ya Mbugani na Kulia ni Ally Kashumali ambae ni Katibu wa Wazee Mbugani.
Wazee Kata ya Mbugani
Mzee Kata ya Mbugani akitoa Mawazo yake ya kuimarisha Umoja ndani ya CCM.
Kijana Kata ya Mbugani akitoa Mawazo yake ya kuimarisha Umoja ndani ya CCM.
Kijana Kata ya Mbugani akitoa Mawazo yake ya kuimarisha Umoja ndani ya CCM.
Kijana Kata ya Mbugani akitoa Mawazo yake ya kuimarisha Umoja ndani ya CCM.
Kijana Kata ya Mbugani akitoa Mawazo yake ya kuimarisha Umoja ndani ya CCM.
Mzee Kata ya Mbugani
Mzee Kata ya Mbugani
Wazee na Vijana Kata ya Mbugani
Wazee na Vijana Kata ya Mbugani
Wazee Kata ya Mbugani
Wanahabari
Ahsante Kwa Kutembea Mtandao Wetu, Endelea Kuwa Nasi.
Powered by Blogger.