LIVE STREAM ADS

Header Ads

MWANZA WATAKIWA KUCHANGIA MAHITAJI YA POLISI JAMII ILI KUIMARISHA ULINZI NA USALAMA.

Wa kwanza Kulia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara ndogondogo katika Masoko na Minada kwa Wilaya za Nyamagana na Ilemela Justine Sagara akifuatiwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishina Msaidizi wa Polisi Charles Mkumbo pamoja na Viongozi wa Jeshi la Polisi hilo katika kilele cha mafunzo ya polisi jamii kwa wanachama wa jumuiya hiyo kilichofanyika jana katika Uwanja wa Magomeni Kirumba Wilayani Ilemela.
Na:George GB Pazzo
Wananchi Mkoani Mwanza Wametakiwa Kushirikiana kwa ukamilifu na Vikundi mbalimbali vya Ulinzi shirikishi, ili kuhakikisha kuwa Wanadumisha amani na Usalama katika maeneo yao.

Rai hiyo ilitolewa jana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Kamishina Msaidizi wa Polisi Charles Mkumbo, wakati akifunga mafunzo ya Polisi Jamii yaliyotolewa kwa Wanachama wa Jumuiya wa Wafanyabiashara ndogondogo katika Masoko na Minada kwa Wilaya za Nyamagana na Ilemela.

Kamanda Mkumbo alisema kuwa wananchi wanao wajibu wa kuendelea kudumisha amani, ulinzi na Usalama uliopo hapa nchini ikiwa ni pamoja na kusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazovikabili vikundi vya polisi jamii.

“Kwa mapungufu mbalimbali kama mlivyosema kuwa mnakabiriwa na ukosefu wa sare, filimbi na sare nawasihi wananchi wasisite kuhamasishana ili kuchangia kwa mfumo wa harambee ili kuyatatua mapungufu hayo badala ya kutegemea serikali au jeshi la polisi pekee”. Alisema Kamanda Mkumbo.

Kwa Upande wake Mkufunzi wa Mafunzo hayo Sajenti wa Polisi Mkoani Mwanza Clement Kabatila alisema kuwa wahitimu wa mafunzo hayo wamefundishwa Uzalendo, Ukakamavu, nidhamu pamoja na utii ambavyo vitawasaidia katika kupambana na uhalifu katika jamii.

Nae Mwenyekiti wa Umoja huo Justin Sagara aliwataka wanachama waliohitimu mafunzo hayo kutimiza majukumu yao kwa utii  na usawa na kwamba atakaebainika kukiuka maadili ya kazi yake Umoja huo utamchukulia hatua kali za kinidhamu.

“Nawaomba mkafanye kazi kwa utii, mkatende haki na kuheshimu sheria bila kumuonea machinga. Na naomba niwaambie kwamba askari yeyote ambae hatakuwa mtii hatafanya kazi minadani kwani tutamuondoa kufanya kazi na sisi”. Alisisitiza Sagara.

Jumla ya Wanachama 34 wanawake wakiwa ni wawili kati ya 50 kutoka Jumuiya hiyo ya Wafanyabiashara ndogondogo katika Masoko na Minada kwa Wilaya za Nyamagana na Ilemela ambao walianza mafunzo ya Polisi jamii mwezi wa pili mwaka huu wamehitimu mafunzo hayo, ambapo katika risala yao wameomba kusaidiwa vitendea kazi ikiwemo pingu, filimbi, tochi pamoja na sare kwa ajili ya kuimarisha ulinzi na usalama katika maeneo yao ya biashara pamoja na majumbani.
TAZAMA PICHA HAPA

No comments:

Powered by Blogger.