CHAMA CHA ACT WAZALENDO CHABAINISHA AINA YA VIONGOZI WANAOHITAJIKA NCHINI.
Mgombea Ubunge wa Chama cha Alliance For Change and Transparency ACT Wazalendo katika Jimbo la Ilemela Mkoani Mwanza Mkiwa Adam Kimwanga (Kushoto) akiwa pamoja na Meneja Kampeni wake Pendo Ojijo (Kulia)
Na:George GB Pazzo
Chama
cha Alliance For Change and Transparency ACT Wazalendo Wilaya ya Ilemela Mkoani
Mwanza kimewataka Watanzania kuwachagua Viongozi watakaoisimamia Tanzania
katika misingi ya Utu, Uzalendo pamoja na Uadilifu katika Uchaguzi Mkuu
unaotarajiwa kufanyika Agost 25 mwaka huu.
Hayo yalisemwa juzi Mgombea Ubunge wa Chama
hicho katika Jimbo la Ilemela Mkiwa Adam Kimwanga alipokuwa akiomba kura kwa
wakazi wa Kata ya Nyamanoro jimboni humo na kuongeza kuwa ACT Wazalendo ndicho
chama pekee nchini chenye viongozi wa aina hiyo.
Kimwanga ambae kwa awamu zote mbili za uongozi wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete alikuwa Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mwanza kupitia Chama cha Wananchi CUF kabla ya kuhamia ACT Wazalendo alibainisha kuwa akipata ridhaa ya kuwa
Mbunge wa Jimbo hilo atahakikisha anasimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo
ikiwemo kutatua kero ya Maji, kukamilisha ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Ilemela, kushughulikia kero na changamoto za elimu pamoja na kuwawezesha akina mama na vijana ili
waweze kujikwamua kiuchumi kupitia ajira shirikishi.
No comments: