LIVE STREAM ADS

Header Ads

JUMAC YAANDAA CHAKULA CHA HISANI JIJINI MWANZA KUSAKA MILIONI 200.

Viongozi wa Jumuiya ya Maendeleo ya Watoto Yatima (JUMAC) wakiwa katika Mkutano na Wanahabari Jijini Mwanza.
Na:George GB Pazzo
Jumuiya ya Maendeleo ya Watoto Yatima Zanzibar JUMAC inatarajia kuendesha harambee Jijini Mwanza kwa malengo ya kuchangisha fedha ili kusaidia katika kukamilisha ujenzi wa shule na zahanati kwa ajili ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu na hatarishi wakiwemo yatima na wenye ualibino katika Mji wa Pemba Zanzibar.

Hayo yalibainishwa jana na Mratibu wa Jumuiya hiyo Joseph Sinde Magutu wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Mwanza kuhusiana na harambee hiyo na kuongeza kuwa matarajio ni kukusanya zaidi ya shilingi milioni 200 zitakazosaidia kufikia malengo hayo.

Magutu alibainisha kuwa JUMAC kwa kushirikiana na Chama cha Albino Mkoa wa Mwanza imeandaa chakula cha hisani ili kukamilisha harambee hiyo ambayo inatarajiwa kufanyika kesho katika Ukumbi wa Gold Crest Hotel kuanzia majira saa moja jioni.

Wadau mbalimbali wakiwemo Wananchi, mashirika pamoja na taasisi za serikali na binafsi wanaombwa kushiriki katika harambee hiyo ili kusaidikia kufikia malengo yake ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo.
Katibu wa JUMAC Joseph Sinde Mabutu
Kaimu Mwenyekiti wa JUMAC Ramadhan Issa Kipaya
Amuru Abdallah Juma kutoka JUMAC
Mkutano wa Viongozi wa JUMAC na Wanahabari Jijini Mwanza

No comments:

Powered by Blogger.