HOTUBA YA DKT. SLAA YATIBUA MAMBO. VIJANA WA UKAWA JIJINI MWANZA WAJIUNGA NA CCM.
Vijana wa Ukawa waliokusanyika hii leo Jijini Mwanza kuunga mkono hotuba ya Dkt.Slaa aliyoitoa jana akitangaza kuanchana na siasa. Vijana hao wametangaza kujiunga na CCM.
Na:Binagi Media Group
Siku
moja baada ya aliekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema
Dkt.Wilbroad Slaa kutangaza kuachana na Siasa, Vijana kutoka Vyama
vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi Ukawa Jijini Mwanza wameandamana na kutangaza
kuachana na Vyama vyao na kujiunga na Chama cha Mapinduzi CCM.
Wakizungumza hii leo katika Viwanja vya Ghandh
Hall Jijini Mwanza walipokuwa wamekusanyika,
Vijana hao wamesema kuwa wameamua kujiunga na CCM ili kuungana na
Dkt.Slaa kupinga maamuzi yaliyochukuliwa na Viongozi wa Chadema katika
kumsimamisha mgombea Urais ambae awali alikuwa akituhumiwa na kashfa za ufisadi.
Vijana hao Wameongeza kuwa hawako tayari
kutumika kisiasa baada ya kubaini kwamba maamuzi yaliyochukuliwa na Mwenyekiti
wa Chadema Freeman Mbowe pamoja na Vyama vya Ukawa ya kumsimamisha Edward
Lowasa kuwa Mgombea Urais hayakuwa sahihi na kwamba hatua inaashiria kuwa
viongozi hao walinunuliwa.
Jana Dkt.Wilbroad Slaa alitangaza mbele ya
Waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam kuachana na Siasa baada ya
kutokubaliana na maamuzi ya Viongozi wenzake ya Kumteua Edward Lowasa Kuwa
Mgombea Urais wa Chadema kupitia Ukawa.
Vijana wa Ukawa waliokusanyika hii leo Jijini Mwanza kuunga mkono hotuba ya Dkt.Slaa aliyoitoa jana akitangaza kuanchana na siasa. Vijana hao wametangaza kujiunga na CCM.
Vijana wa Ukawa waliokusanyika hii leo Jijini Mwanza kuunga mkono hotuba ya Dkt.Slaa aliyoitoa jana akitangaza kuanchana na siasa. Vijana hao wametangaza kujiunga na CCM.
Binagi Media Group, Kwa Pamoja Tuijuze Jamii
No comments: