LIVE STREAM ADS

Header Ads

WATUMIAJI WA MITANDAO YA KIJAMII NCHINI WATAHADHARISHWA.

Na:George GB Pazzo
Chama cha Waandishi wa Habari wanaopiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uhalifu nchini Ojadact kimewatahadharisha watumiaji wa Mitandao ya Kijamii kujihadhari na Matumizi ya Mitandao yasiyo sahihi ili kuepuka kukumbwa na sheria ya makosa ya mtandaoni ya mwaka 2015.

Tahadhari hiyo ilitolewa jana Jijini Mwanza na Mwenyekiti wa Chama hicho Edwin Soko alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya sheria hiyo ambayo imeanza kutumika rasmi hiyo jana.

Soko amewahimiza watumiaji wa Mitandao mbalimbali ya kijamii kujiepusha na suala la usambazaji wa picha za utupu, matusi pamoja na ujumbe wenye viashiria vya uchochezi kwa kuwa hayo ni miongoni mwa mambo yanayokinzana na sheria hiyo.

Miongoni mwa adhabu anazoweza kukabiliana nayo mtumiaji wa mitandao ya kijamii anaekiuka sheria hiyo ya Makosa ya Mitandaoni ya mwaka 2015 ni pamoja na kufungwa gerezani katika kifungo cha hadi miaka 10 ama kulipa faini ambayo inafikia hadi shilingi Milioni 30.

Wakati sheria hiyo inaanza kufanya kazi hii leo, baadhi ya watumiaji wa mitandao mbalimbali ya Kijamii ikiwemo Blog, facebook na whatsupp wameeleza kuwa ujio wake unaweza kukandamiza uhuru wa Watanzania kutoa na kupata taarifa kwa njia ya mitandao huku wengine wakisema kuwa itasaidia kuimarisha matumizi sahihi ya Mitandao hiyo.
BONYEZA PLAY HAPA CHINI KUSIKILIZA

No comments:

Powered by Blogger.