LIVE STREAM ADS

Header Ads

OJADACT YAZIDI KULIA NA SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAONI AMBAYO IMEANZA KUTUMIKA LEO.

Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanaopiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uharifu nchini OJADACT Edwin Soko akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ofisi za Chama hicho zilizopo Jijini Mwanza juu ya Sheria ya Makosa ya Mtandaoni ilioanza kutumika Rasmi hii leo hapa nchini.
 Picha na George GB Pazzo
Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari nchini.
Sheria ya makosa ya jinai ya kimtandao   2015…1/9/2015…Jengo la CCM Mkoa wa Mwanza.

Ndugu  waandishi wa  habari  tumewaita  hapa  kwa ajili  ya  kuongea  nanyi  juu  ya  kuanza  rasmi hii  leo  kutumika kwa  sheria   ya  makosa  ya kimtandao  na ile  ya  miamala  ya  kielektoniki.

Sheria  ya  makosa ya  mtandaoni kwa  ujumla  inaainisha makosa   yanayohusiana na matumizi ya  mfumo wa kompyuta  na  teknolojia  ya  habari na mawasiliano, na kuweka  utaratibu  wa upelelezi, ukusanyajina matumizi  ya  ushahidi  wa kieletroniki.

OJADACT   kwanza  tunaipongeza  serikali  kuleta  sheria  hii ili kuendana na kasi  ya  kukua  kwa teknolojia  na kuongezeka  kwa  vitendo  vya  kihalifu Tanzania.

UCHAMBUZI WETU JUU YA SHERIA HII Uzuri wa sheria hii.
(1)Sheria hii bado ina tija kubwa ya  kuthibiti vitendo vya uhalifu wa kimtandao kama kutuma picha za ngono, wizi wa fedha,  kuandika uchochezi,kuandika matuzi na kuzusha taarifa za uongo, kusababisha ajali na nyinginenzo.

(2)Sheria hii ina nafasi kubwa katika kulinda maadili ya taifa, hasa kwa kutoruhusu sasa  matusi, uongo na uzushi kuwekwa mtandaoni.

Changamoto  za  sheria  hii
(1)Sheria hii itafanya Nchi kuwa adui wa  matumizi ya mtandao na teknolojia ya habari na mawasiliano kutokana na muundo wa sheria husika.

(2)Sheria inaminya uhuru wa mawasiliano  mtandaoni ilivyobainishwa kwenye sheria mama  ya Nchi ambayo ni katiba, kwani hata jambo  ambalo ni la kweli lakini likitafsiriwa ni  uzushi au uongo basi mtoa taarifa atashughulikiwa na hivyo itapelekea watu wengi kuogopa kutoa taarifa yoyote ile.

(3)Sheria hii itahitaji zaidi mchango wa kimahakama katika kuamua kipi ni kosa na kipi sio kosa kwa mujibu wa sheria kati ya mtoa  taarifa na mpokeaji taarifa na mazingira ya  taarifa hiyo.

(4)Sheria pia inahitaji mchango mkubwa wa kitafsiri kwani neno matusi yanaweza kuwa na  mgongano mkubwa na maana ya kimaudhui, ambayo yanaweza pia kuonekana sio matusi.
Mambo ya kuepuka ili kuwa salama na  sheria hii
·Epuka kusambaza ujumbe wa uchochezi ama  ushawishi
·Epuka kusambaza au kutunga ujumbe  unaoleta uchochezi
·Epuka kusambaza picha chafu/utupu
·Epuka wizi wa kupitia mitandao
·Epuka kushiriki kumchafua mtu
·Epuka kupoteza simu bila kutoa taarifa
·Epuka kumpatia mtu lini yako ya simu

Ndugu waandishi wa habari tunawaomba sana kuwa makini na sheria hii na pia  kuihabarisha jamii kuwa makini pia na sheria  hii kwa lengo la kutoishia gerezani au  kulipa au vyote kwa pamoja.        
Imetolewa na;
Edwin Soko

Mwenyekiti Ojadact
Mwenyekiti wa Ojadact Edwin Soko
Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanaopiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uharifu Nchini OJADACT Edwin Soko akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ofisi za Chama hicho zilizopo Jijini Mwanza juu ya Sheria ya Makosa ya Mtandaoni ilioanza kutumika Rasmi hii leo hapa nchini.

No comments:

Powered by Blogger.