LIVE STREAM ADS

Header Ads

SIKU YA WAHANDISI NCHINI, WATANZANIA WATAKIWA KUJENGA IMANI NA WAKANDARASI WAZALENDO.

Jengo la Kibiashara linalojengwa na Kampuni ya Kigeni Jijini Mwanza.
Na:George GB Pazzo
Watanzania wameshauriwa kujenga imani na Wakandarasi wa ndani ya nchi na hivyo kutoa tenda za ujenzi kwa Makampuni ya kizalendo badala ya kuwategemea wakandarasi kutoka nje ya nchi.

Ushauri huo umetolewa hii leo Jijini Mwanza na Mkurugenzi wa Kampuni ya Ujenzi ya JBM Civil Contractors Joseph Castus wakati akizungumza na Radio Metro juu ya Siku ya Wahandisi nchini iliyoadhimishwa Jijini Dar es salaam.

Castus amesema kuwa Serikali pamoja na Wananchi wanapaswa kutambua kuwa wapo Wakandarasi bora nchini ambao wana uwezo wa kujenga na kusimamia miradi mikubwa ya ujenzi hivyo tenda zinapotangazwa vipaumbele zaidi vitolewe kwa Wakandarasi hao.

Pia meongeza kuwa Bodi za zabuni nchini bado hazijawa na imani juu ya Wakandarasi wa ndani kutokana na Wakandarasi wengi kukabiliwa na uhaba wa mitaji hatua ambao husababisha wakandarasi wa kigeni kupewa miradi mingi ya ujenzi ambapo ameomba Serikali kuwawezesha Wakandarasi hao kupitia Mikopo yenye riba nafuu.

Maadhimisho ya Siku ya Wahandisi nchini yameanza hii leo na yanatarajia kufikia tamati kesho ambapo yamekuwa ni maadhimisho ya 13 tangu kuzinduliwa kwake mwaka 2003 yakiwa yamelenga kuiwezesha jamii kutambua michango tunu inayofanywa na wahandisi wa Tanzania katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi pamoja na kuwahamasisha vijana kusoma taaluma ya uhandisi.

No comments:

Powered by Blogger.