LIVE STREAM ADS

Header Ads

BODABODA JIJINI MWANZA WATAKIWA KUWEKA SIASA KANDO.

Na:George Binagi-GB Pazzo
Waendesha pikipiki maarufu kwa jina la bodaboda Mkoani Mwanza, wamehimizwa kuweka kando itikadi zao za kisiasa na kujikita zaidi kwenye majukumu yao ya kazi badala ya siasa kwa kuwa masuala ya uchaguzi mkuu tayari yamefikia tamati.

Rai hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Muungano wa Waendesha Pikipiki Mkoani Mwanza Makoye Kayanda, wakati akizungumza na Binagi Radio Habari ya Binagi Media Group.

Makoye alisema kuwa uchaguzi umekamilika hivyo maisha yanapaswa kuendelea kwa kila mmoja kufanya kazi kwa bidii katika eneo lake huku akisahau yale yote yaliyojitokeza katika mchakato mzima wa Uchaguzi Mkuu.

“Tumemaliza Uchaguzi salama hivyo niwashukuru waendesha pikipiki kwa hilo na kila mmoja aendelee kufanya kazi kwa bidii zaidi kwani maisha ni kazi”. Amesema Kayanda.

Aidha alitoa rai kwa watumiaji wa barabara wakiwemo bodaboda, kuzingatia suala la Usalama barabarani ikiwa ni pamoja na kuzingatia utii wa sheria bila shuruti.

Katika harakati za Uchaguzi Mkuu mwaka huu, waendesha pikipiki kote nchini walionekana kuwa na msukumo mkubwa wa kuambatana na wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi, pindi walipokuwa katika harakati za kuomba kura kwa wananchi.
SIKILIZA RIPOTI KAMILI KUPITIA BINAGI RADIO

No comments:

Powered by Blogger.